Posts

Showing posts from January, 2018

DUNIA UWANJA WA FUJO-RIWAYA

Dunia Uwanja wa Fujo  ni  riwaya  iliyoandikwa na  Euphrase Kezilahabi  mwaka wa  1975 . Ni riwaya ambayo inasawili  maisha  ya wanadamu  hususani waishio  Afrika Mashariki , hasa hasa katika nchi ya  Tanzania . “Dunia Uwanja wa Fujo” inaelezea jinsi maisha yaliyopo  duniani  ni sawasawa na fujo, kwani kila mtu anayekuja duniani huleta fujo zake na baadaye kutoweka.  Mwandishi anaelezea kwamba kila mtu anafanya fujo zake na kusababisha matatizo mbalimbali katika  jamii  yake kama vile  mauaji ,  ukabila , umalaya ,  uchawi ,  ubakaji ,  ulevi  wa kupindukia n.k. Hivyo basi mwandishi anaamini kwamba katika  dunia  kila mtu anakuja na fujo zake na kutoweka. Kwa mfano,  mhusika  Tumaini katika riwaya hii ameleta fujo zake kama vile umalaya, mauaji na mengine mengi na baadaye kutoweka. MBINU ZA KIFANI Fani za kijadi ndizo zilizosababisha riwaya izalike. "Dunia ni Uwanja wa Fujo” ni mojawapo ya riwaya zilizotokana na fani ya kijadi ambayo ni  sira . Sira ni fani ya kijadi ambay