Skip to main content

tofauti kati ya muhtasari wa 2005 na ule wa 2010



Muhtasari, ni ufundisho wa mambo yanayofundishwa katika shule au chuo, vidokezo vya somo. (J.S.Mdee, K. Njogu, Shati A. 2011).
Muhtasari, ni muongozo unaotaja mambo yote yatakayofundishwa, mbinu za ufundishaji, na zana za kufundishia.
Mhtasari wa somo, ni mwongozo unaotaja mambo yatakiwayo kufundishwa kwa kipindi maalumu.
Aidha muhtasari wa somo la Kiswahili huwa na muundo yaani utangulizi, malengo ya elimu Tanzania, malengo ya elimu ya sekondari, ujuzi wa jumla wa somo la Kiswahili katika shule za sekondari, malengo ya jumla ya kufundisha somo la Kiswahili katika shule za sekondari, ujuzi, malengo na majedwali ya ufundishaji kidato cha 1 – 4.
Tofauti, ni ile hali ya kutofanana au kutokuwa sawa. Tofauti inapatikana kwa kuangalia umbo la kitu, hali ya kitu, kazi ya kitu na hata muda. Tofauti zimejitokeza katika upande wa utangulizi, ujuzi, na malengo.
Zifuatazo ni tofauti zilizojitokeza katika muhtasari wa mwaka 2005 na muhtasari wa mwaka 2010, katika kipengele cha utangulizi:-
Utangulizi, katika kipengele cha utangulizi, muhtasari wa mwaka 2005 wametumia neno muhamo wa ruwaza wakibainisha vipengele au mambo yaliozingatiwa katika muhtasari huu. Lakini katika muhtasari wa mwaka 2010 wametumia neno mbinu shirikishi katika kipengele hichohicho kinachopambanua mambo au vipengele vilivyozingatiwa katika muhtasari huo. Maneno yote hayo mawili yaani muhamo ruwaza na mbinu shirikishi yana maana inayofanana ambayo ni kuwashirikisha wanafunzi katika tendo la ufundishaji na ujifunzaji.
Uandishi wa muhtasari, katika muhtasari wa mwaka 2010 umetajwa vizuri katika jalada la nje kuwa ni muhtasari wa mwaka 2010 lakini ndani yake katika ukurasa wa iv kwenye kipengele cha utangulizi kuna kosa la kiuandishi au kiuchapaji ambapo umetajwa kama muhtasari wa mwaka 2005. Hii inaashiria kuwa kulikuwa na uzembe wakati wa uhariri.
Ushauri wa mwalimu, kwenye muhtasari wa mwaka 2005 mwalimu anashauriwa kuwa anaweza kutumia kitabu cha kiada zaidi ya kimoja ili kujiongezea maarifa na kumrahisishia ufundishaji, lakini katika muhtasari wa mwaka 2010 mwalimu ameshauriwa azingatie kuwa “Orodha ya vitabu vya kufundishia Kiswahili vitakuwa vikitolewa na wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi. Muhtasari huu wa mwaka 2010, umemfanya mwalimu kama mtu wa kusubilia tu pasipo kujishughulisha na usomaji wa vitabu tofauti tofauti ili kuongeza maarifa katika somo la Kiswahili.
Muhtasari huu wa mwaka 2005 na muhtasari wa mwaka 2010, umetofautiana katika mambo machache sana tukizingatia vipengele tofauti tofauti vya muhtasari. Lakini pia muhtasari wa mwaka 2010 na muhtasari wa mwaka 2005 umefanana kwa asilimia nyingi ukilinganisha na kutofautiana kwake. Muhtasari huu wa 2005 na 2010 umefanana katika muda wa kufundishia, malengo ya elimu Tanzania, madhumuni ya elimu ya sekondari, ujuzi wa somo la Kiswahili, malengo ya jumla ya kufundisha somo la Kiswahili kwa shule za sekondari, muundo wa muhtasari, ujuzi wa kila kidato, malengo ya kila kidato, mada za kila kidato, idadi ya vipindi na masaa.















                                        MAREJELEO
Ø  J.S.Mdee, K. Njogu, Shati A. (2011). Kamusi ya karne ya 21: Longhorn.
Ø  Muhtasari wa Kiswahili kwa shule za sekondari, kidato cha i-iv (2005).
Ø  Muhtasari wa Kiswahili kwa shule za sekondari, kidato cha i-iv (2010).

Comments

Popular posts from this blog

KISWAHILI FORM 1: FASIHI SIMULIZI

KISWAHILI Form 1 Topic 4 FASIHI SIMULIZI Fasihi simulizi ni moja kati ya tanzu za fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo. Katika mada hii utajifunza na kisha utaweza kubainisha tanzu na vipera vya fasihi simulizi pamoja na ufafanuzi wake. Na pia utaweza kutofautisha kati ya kipera na kipera au kati ya utanzu na utanzu. Ubainishaji wa Tanzu za Fasihi Simulizi Tanzu za Fasihi Simulizi Bainisha tanzu za fasihi simulizi Fasihi Simulizi ni kazi ya fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo kama vile; hadithi, ngoma na vitendawili. Tanzu za Fasihi Simulizi ni pamoja na hizi zifuatazo: Masimulizi/hadithi Semi Ushairi Mazungumzo Maigizo Ngomezi Ufafanuzi wa Vipera vya Tanzu za Fasihi Simulizi Vipera vya Hadithi Fafanua vipera vya hadithi SIMULIZI/ HADITHI Masimulizi ni fasihi yenye kusimulia habari fulan...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

Mbinu za kufundishia , ni miongozo mbalimbali atumiayo mwalimu wakati wa kufundisha somo aliloliandaa kwa wanafunzi wake. Walimu wanapaswa kuamua kwa kuchagua kwa makini njia na mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Ziko njia nyingi za kutengeneza mazingira ya mtoto aweze kujifunza na pia ziko mbinu nyingi za kufundishia. Pamoja na wingi huo tunaweza kuzigawa katika makundi makuu mawili kadri ya jinsi zinavyowashirikisha watoto katika tendo la kujifunza, ambazo tunaweza kuziita shirikishi na zisizo shirikishi . Zifuatazo ni baadhi ya mbinu shirikishi na zisizo shirikishi za kufundishia pamoja na faida na hasara zake:- Njia ya majadiliano , njia hii imekuwa ikitumika katika ufundishaji kwa muda mrefu. Katika kujadiliana mwanafunzi mmoja mmoja hupata nafasi ya mawazo aliyonayo kuhusu suala linalojadiliwa na yeye pia huweza kupata mawazo yaw engine. Katika majadiliano mwanafunzi hupata ujuzi mpya nje na ule aliokuwa nao kabla hajashiriki kat...

DHANA YA USHAIRI ILIVYOFAFANULIWA NA WATAALAMU MBALIMBALI

Ushairi kama moja kati ya tanzu za fasihi inayowasilishwa katika namna zote aidha kwa lugha ya maandishi au kwa lugha ya masimulizi una mchango au nafasi kubwa sana katika kunufaisha au kustawisha maisha ya binadamu kwa kumuelimisha, kumsisimua, kutunza na kuhifadhi amali zake pamoja na kukuza na kuendeleza lugha yake kama moja kati ya vipengere muhimu maishani mwake. Ushairi kama nudhumu katika fasihi simulizi hujumuisha nyimbo, ngonjera, tenzi na mashairi yenyewe. Ushairi wa Kiswahili waweza kuainishwa katika tanzu au katika kumbo mbalimbli kama asemavyo Mulokozi (1996) kuwa zipo kumbo kuu tatu ambazo ni ushairi wa kijadi au kimapokeo, ushairi wa mlegezo au huru na ushairi wa maigizo. Wanazuoni wafuatao wa mashairi ya kimapokeo wametoa maana za ushairi kama ifuatavyo:- Shaaban Robert (1958:37). “Ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi. Zaidi ya kuwa na sanaa ya vina, ushairi una ufasaha wa maneno machache au muhtasari…, mawazo, maoni na fikra za ndani zi...