Skip to main content

KISWAHILI FORM 4: KUONGEZA MSAMIATI WA KISWAHILI

KISWAHILI Form 4 Topic 1

KUONGEZA MSAMIATI WA KISWAHILI
Lugha hukua na kubadilika kila wakati kulingana na maendeleo ya jamii. Kigezo kimojawapo cha kukua na kubadilika kwa lugha ni kuongezeka kwa msamiati. Ili msamiati uongezeke katika lugha sharti maneno mapya yaundwe.
Njia za Uundaji Maneno
Elezea njia mbalimbali za uundaji maneno
Uundaji wa Msamiati hutokea kwa njia mbalimbali zifuatazo:
  1. Kubadili mpangilio wa herufi.
  2. Kuambatanisha maneno.
  3. Kutohoa maneno ya lugha nyingine.
  4. Uambishaji wa maneno.
  5. Kufanikisha sauti, umbo, mlio na sura.
Kuunda msamiati kwa kubadili mpangilio wa herufi
Neno hujengwa kwa vitamkwa au herufi. Neno jipya lenye maana tofauti huweza kuundwa kwa kubadili mpangilio wa neno lingine
Example 1
Mfano
  • Neno lima, lina herufi l, i, m, a, herufi hizi huweza kujenga maneno kama mali, kumi,imla, mila.
  • Neno tua lina herufi t, u, a, herufi hizi zina weza kujenga maneno kama:- tatu, tua, viatu, tatua.
Njia ya kuambatanisha maneno
Kuna njia tatu za kuambatanisha meneno
Njia ya kurudufisha au kukariri neno
Mfano; barabara, sawasawa, polepole, katikati, vilevile.
Njia ya uundaji wa Msamiati kwa kuunganisha maneno mawili tofauti
Nomino na Nomino
  • Punda + mlia unapata Pundamilia
  • Bibi + Shamba unapata Bibishamba
  • Afisa + Elimu unapata Afisaelimu
  • Mwana + Siasa unapata Mwanasiasa
  • Bata + maji unapata Batamaji
Kuunganisha kitenzi na Nomino/Jina
  • Changa + moto changamoto
  • Chemsha + bongo chemshabongo
  • Piga + mbizi pigambizi
  • Zima + moto zimamoto
Kuunganisha maneno mawili na kudondosha baadhi ya herufi
Example 2
Mfano
  • Baraza la Kiswahili Tanzania BAKITA
  • Mzaliwa wa mahali Fulani MZAWA
  • Chama cha Mapinduzi CCM
  • Nyamamfu NYAMAFU
Kutohoa maneno kutoka lugha nyingine
Kila lugha na tabia ya kuchukua maneno lugha nyingine ili kukidhi mahitaji ya Msamiati. Maneno kutoka lugha nyingine yanapoteuliwa hubadilishwa kimatamshiili ya fuate kanuniza Kiswahili.
Maneno yanayotoholewa kutoka lugha nyingine husanifishwa na asasi za lugha ya Kiswahili ndipo ya ruhusiwe kutumiwa rasmi.
Example 3
Mfano
Neno la KiswahiliLugha ya MwanzoNeno Lililotoholewa
KijerumaniSchule
SalamaKiarabuSalaam
DukaKihindiDukan
KarotiKiingerezaCarrot
ShatiKiingerezaShirt
PichaKiingerezaPicture
PapaiKihispaniaPapaya
MezaKirenoMezi
ShukraniKiarabuShukran
NgeliKihayaEngeli
IkuluKinyamweziIkulu
Ng'atukaKizanakiNg'atuka
NdafuKichagaNdafu
Namba
Kuunda maneno kwa njia ya uambishaji wa maneno
Hii ni njia ya kubandika viambishi awali na tamati kwe nyekiini. Ujenzi wa maneno hutokana na mzizi mmoja kuonesha maana tofauti ingawa maana zina husiana.
Mfano mzizi: -lim-.Tukipachika viambishi awali na tamati tunapata maneno kama lima, analima, walilima, kilimo, limiana,halitalimwa na ukulima.
Kufananisha sauti, sura au tabia
Example 4
Mfano
  • Kengele - utokana na sauti ya kengele inapo pigwa
  • Pikipiki - hutokana na muungurumo wa pikipiki
  • Ndizi mkono wa tembo – Ndizi inayo fananishwa na mkono wa mnyama tembo
  • Chubwi - Jiwe au chura atumbukiapo katika kina cha maji.
Mazingira yanayoelezea Kuhitaji Maneno Mapya
Elezea mazingira yanayoelezea kuhitaji maneno mapya
Mabadiliko mengi yanatokea kila siku katika nyanja mbalimbali za kimaisha-mabadiliko ya kiuchumi, kisiasa, kisayansi na kiteknolojia. Katika mazingira kama haya, watu watahitaji kuwasiliana, lugha itahitaji kuunda maneno ili kuwasilisha dhana mpya zilizoibuka. Kwa mfano, maneno kama vile nywila, kisakuzi, udukuzi, puku, talakirishi n.k yameundwa ili kuwasilisha dhana za kiteknoljia kwa Kiswahili.
Undaji wa Maneno katika Miktadha mbalimbali
Unda maneno katika miktadha mbalimbali
Mabadiliko ya kimaendeleo yanafanya lugha ihitaji maneno ya kuyafikisha na kutumiwa na jamii. Ili kukidhi mahitaji hayo, maneno mapya yanazuka. Maneno hayo yanaweza kuwa katika fani mbalimbali, kama vile sayansi na teknolojia, siasa, utamaduni na uchumi kulingana na mkondo wa maendeleo. Mfano wa msamiati ni kama vile fedha, ushuru, kumpyuta, ukoloni, hospitali, suruali n.k
Activity 1
Unda maneno katika miktadha mbalimbali. 

Comments

Popular posts from this blog

DHANA YA USHAIRI ILIVYOFAFANULIWA NA WATAALAMU MBALIMBALI

Ushairi kama moja kati ya tanzu za fasihi inayowasilishwa katika namna zote aidha kwa lugha ya maandishi au kwa lugha ya masimulizi una mchango au nafasi kubwa sana katika kunufaisha au kustawisha maisha ya binadamu kwa kumuelimisha, kumsisimua, kutunza na kuhifadhi amali zake pamoja na kukuza na kuendeleza lugha yake kama moja kati ya vipengere muhimu maishani mwake. Ushairi kama nudhumu katika fasihi simulizi hujumuisha nyimbo, ngonjera, tenzi na mashairi yenyewe. Ushairi wa Kiswahili waweza kuainishwa katika tanzu au katika kumbo mbalimbli kama asemavyo Mulokozi (1996) kuwa zipo kumbo kuu tatu ambazo ni ushairi wa kijadi au kimapokeo, ushairi wa mlegezo au huru na ushairi wa maigizo. Wanazuoni wafuatao wa mashairi ya kimapokeo wametoa maana za ushairi kama ifuatavyo:- Shaaban Robert (1958:37). “Ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi. Zaidi ya kuwa na sanaa ya vina, ushairi una ufasaha wa maneno machache au muhtasari…, mawazo, maoni na fikra za ndani zi...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

Mbinu za kufundishia , ni miongozo mbalimbali atumiayo mwalimu wakati wa kufundisha somo aliloliandaa kwa wanafunzi wake. Walimu wanapaswa kuamua kwa kuchagua kwa makini njia na mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Ziko njia nyingi za kutengeneza mazingira ya mtoto aweze kujifunza na pia ziko mbinu nyingi za kufundishia. Pamoja na wingi huo tunaweza kuzigawa katika makundi makuu mawili kadri ya jinsi zinavyowashirikisha watoto katika tendo la kujifunza, ambazo tunaweza kuziita shirikishi na zisizo shirikishi . Zifuatazo ni baadhi ya mbinu shirikishi na zisizo shirikishi za kufundishia pamoja na faida na hasara zake:- Njia ya majadiliano , njia hii imekuwa ikitumika katika ufundishaji kwa muda mrefu. Katika kujadiliana mwanafunzi mmoja mmoja hupata nafasi ya mawazo aliyonayo kuhusu suala linalojadiliwa na yeye pia huweza kupata mawazo yaw engine. Katika majadiliano mwanafunzi hupata ujuzi mpya nje na ule aliokuwa nao kabla hajashiriki kat...

DHANA YA MATUMIZI YA LUGHA, REJESTA, UTATA

Matumizi ya lugha ni namna ambavyo wazungumzaji wa lugha hutumia lugha kwa kuzingatia mila, desturi na kaida mbalimbali za jamii inayohusika. Katika mada hii utajifunza mambo ya msingi ya kuzingatia unapotumia lugha. Utaelewa dhana mbalimbali zinazohusishwa na matumizi ya lugha kama vile rejesta, misimu, utatata katika lugha, lugha ya mazungumzo na lugha ya maandishi. Matumizi ya lugha ni namna ambavyo wazungumzaji wa lugha hutumia lugha kwa kuzingatia mila, desturi na kaida mbalimbali za jamii inayohusika. Dhima ya matumizi ya lugha Dhima kuu ya lugha ni kupashana habari, ujuzi na maarifa mbalimbali. Vilevile lugha husaidia kujenga uhusiano mwema baina ya watu. Uhusiano huo unaweza kuwa wa kijamii, kielimu, kibiashara, kihuduma, kisiasa, kiuchumi n.k. Kwa hiyo, kujua jinsi ya kuitumia lugha kama inavyotakiwa, kunasaidia kufikisha vizuri ujumbe unaotakiwa bila kuupotosha. Vilevile kunasaidia kuepuka migongano, hasa ya kijamii kwa kuwa utakuwa umetumia lugha kwa mujibu wa mi...