Skip to main content

SHAIRI: NISEME NINI UJE KWANGU


Kila nikifikiria,ninashindwa kuamua,
Sawa ningevumilia,ila penzi lasumbua,
Kipi sijamwambia,pendo langu kulijua,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Neno nimeshachelewa,lanifanya nikose nguvu,
Hasa ninapogunduwa,kisa ni uvumilivu,
Ni kweli hakuelewa,ishara zangu na wivu,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Sasa nina taabika,na pendo langu hewani,
Si mchezo nateseka,kasema lirudi ndani,
Nashindwa hata kucheka,sipo tena furahani,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Rafiki niseme nini,huyu mtu aje kwangu,
Najua haniamini,atesa fikira zangu,
Mwambie aniamini,mawazo yarudi kwangu.
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Mwambie napenda Mori,sina utani kwa hili,
Leo mie sina gari,kwenye gari siyo mbali,
Nikikosa nina sori,ya kizungu na kiswahili,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Pia mwambie ukweli,wengi wanamtamani,
Hawajui yake hali,wao wapenda kimini,
Tatizo la wake mwili,wakijua hataamini,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Wengi nimeshawaona,wakilia kwa uchungu,
Na ngumu sana kupona,wabaki kusema Mungu,
Sipendi kwake kuona,aje kukufuru Mungu,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Kaditama ninatua,uufikishe ujumbe,
Mie moyo waugua,sina nguvu hata chembe,
Awai kumgundua,yule wake kama wembe,
Ataumizwa na kulizwa,nipo chaguo lake.

Comments

Popular posts from this blog

DHANA YA USHAIRI ILIVYOFAFANULIWA NA WATAALAMU MBALIMBALI

Ushairi kama moja kati ya tanzu za fasihi inayowasilishwa katika namna zote aidha kwa lugha ya maandishi au kwa lugha ya masimulizi una mchango au nafasi kubwa sana katika kunufaisha au kustawisha maisha ya binadamu kwa kumuelimisha, kumsisimua, kutunza na kuhifadhi amali zake pamoja na kukuza na kuendeleza lugha yake kama moja kati ya vipengere muhimu maishani mwake. Ushairi kama nudhumu katika fasihi simulizi hujumuisha nyimbo, ngonjera, tenzi na mashairi yenyewe. Ushairi wa Kiswahili waweza kuainishwa katika tanzu au katika kumbo mbalimbli kama asemavyo Mulokozi (1996) kuwa zipo kumbo kuu tatu ambazo ni ushairi wa kijadi au kimapokeo, ushairi wa mlegezo au huru na ushairi wa maigizo. Wanazuoni wafuatao wa mashairi ya kimapokeo wametoa maana za ushairi kama ifuatavyo:- Shaaban Robert (1958:37). “Ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi. Zaidi ya kuwa na sanaa ya vina, ushairi una ufasaha wa maneno machache au muhtasari…, mawazo, maoni na fikra za ndani zi...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

Mbinu za kufundishia , ni miongozo mbalimbali atumiayo mwalimu wakati wa kufundisha somo aliloliandaa kwa wanafunzi wake. Walimu wanapaswa kuamua kwa kuchagua kwa makini njia na mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Ziko njia nyingi za kutengeneza mazingira ya mtoto aweze kujifunza na pia ziko mbinu nyingi za kufundishia. Pamoja na wingi huo tunaweza kuzigawa katika makundi makuu mawili kadri ya jinsi zinavyowashirikisha watoto katika tendo la kujifunza, ambazo tunaweza kuziita shirikishi na zisizo shirikishi . Zifuatazo ni baadhi ya mbinu shirikishi na zisizo shirikishi za kufundishia pamoja na faida na hasara zake:- Njia ya majadiliano , njia hii imekuwa ikitumika katika ufundishaji kwa muda mrefu. Katika kujadiliana mwanafunzi mmoja mmoja hupata nafasi ya mawazo aliyonayo kuhusu suala linalojadiliwa na yeye pia huweza kupata mawazo yaw engine. Katika majadiliano mwanafunzi hupata ujuzi mpya nje na ule aliokuwa nao kabla hajashiriki kat...

DHANA YA MATUMIZI YA LUGHA, REJESTA, UTATA

Matumizi ya lugha ni namna ambavyo wazungumzaji wa lugha hutumia lugha kwa kuzingatia mila, desturi na kaida mbalimbali za jamii inayohusika. Katika mada hii utajifunza mambo ya msingi ya kuzingatia unapotumia lugha. Utaelewa dhana mbalimbali zinazohusishwa na matumizi ya lugha kama vile rejesta, misimu, utatata katika lugha, lugha ya mazungumzo na lugha ya maandishi. Matumizi ya lugha ni namna ambavyo wazungumzaji wa lugha hutumia lugha kwa kuzingatia mila, desturi na kaida mbalimbali za jamii inayohusika. Dhima ya matumizi ya lugha Dhima kuu ya lugha ni kupashana habari, ujuzi na maarifa mbalimbali. Vilevile lugha husaidia kujenga uhusiano mwema baina ya watu. Uhusiano huo unaweza kuwa wa kijamii, kielimu, kibiashara, kihuduma, kisiasa, kiuchumi n.k. Kwa hiyo, kujua jinsi ya kuitumia lugha kama inavyotakiwa, kunasaidia kufikisha vizuri ujumbe unaotakiwa bila kuupotosha. Vilevile kunasaidia kuepuka migongano, hasa ya kijamii kwa kuwa utakuwa umetumia lugha kwa mujibu wa mi...