Skip to main content

SHAIRI: U WAPI UJITOKEZA

Nakukumbuka kwa jina,kisa mama,alikwita,
Si Jojina Saraphina,Sarah pia aliita,
Mora moja nilikwona,siku kwenu ninapita,
Uwapi ujitokeze,walisema upo Dar.

Nilibadili na njia,kisa kwenu kupapita,
Jina lililipatia,kumbe nawe ulipita,
Wenyeji nawasumbua,hadi mwizi wananita,
U wapi ujitokeze,walisema upo Dar.

Walijua twajuana,hata jina nikakwita,
Sikuwa makini sana,japo moyo ulipwita,
Nilijua ningekwona,nikirudi nakukuta,
U wapi ujitokeze,walisema upo Dar.

Kwa yeyote ajuaye,alipo wangu muhibu,
Aseme alipo yeye,kila swali nitajibu,
Katoka Njombe yeye,mtoto wa baba bubu,
U wapi ujitokeze,walisema upo Dar.

Rangi maji ya kunde,urefu wa wastani,
Nywele lazima upende,kope hadi natamani,
Jino la mbele upande,na kamwanya ka thamani,
U wapi ujitokeze,walisema upo Dar.

Kama umeshaolewa,Sarah sema nitambue,
Nijuwe nimechelewa,ili nisikusumbue,
Mwenzako ni muelewa,sema moyo uamue,
U wapi ujitokeze,walisema upo Dar.
Kama bado njoo kwangu,sina mwingine banati,
Hutoupata uchungu,mwenyewe tapiga goti,
Michepuko nungunungu,hailengwi kwa manati,
U wapi ujitokeze,walisema upo Dar.

Mwisho mama utambue,moyo wangu umependa,
Kwani tangu siku ile,wengine kutwa wadunda,
Na pia nikuambie,wajua kipi wapenda,
U wapi ujitokeze,walisema upo Dar.

Comments

Popular posts from this blog

KISWAHILI FORM 1: FASIHI SIMULIZI

KISWAHILI Form 1 Topic 4 FASIHI SIMULIZI Fasihi simulizi ni moja kati ya tanzu za fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo. Katika mada hii utajifunza na kisha utaweza kubainisha tanzu na vipera vya fasihi simulizi pamoja na ufafanuzi wake. Na pia utaweza kutofautisha kati ya kipera na kipera au kati ya utanzu na utanzu. Ubainishaji wa Tanzu za Fasihi Simulizi Tanzu za Fasihi Simulizi Bainisha tanzu za fasihi simulizi Fasihi Simulizi ni kazi ya fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo kama vile; hadithi, ngoma na vitendawili. Tanzu za Fasihi Simulizi ni pamoja na hizi zifuatazo: Masimulizi/hadithi Semi Ushairi Mazungumzo Maigizo Ngomezi Ufafanuzi wa Vipera vya Tanzu za Fasihi Simulizi Vipera vya Hadithi Fafanua vipera vya hadithi SIMULIZI/ HADITHI Masimulizi ni fasihi yenye kusimulia habari fulan...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

Mbinu za kufundishia , ni miongozo mbalimbali atumiayo mwalimu wakati wa kufundisha somo aliloliandaa kwa wanafunzi wake. Walimu wanapaswa kuamua kwa kuchagua kwa makini njia na mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Ziko njia nyingi za kutengeneza mazingira ya mtoto aweze kujifunza na pia ziko mbinu nyingi za kufundishia. Pamoja na wingi huo tunaweza kuzigawa katika makundi makuu mawili kadri ya jinsi zinavyowashirikisha watoto katika tendo la kujifunza, ambazo tunaweza kuziita shirikishi na zisizo shirikishi . Zifuatazo ni baadhi ya mbinu shirikishi na zisizo shirikishi za kufundishia pamoja na faida na hasara zake:- Njia ya majadiliano , njia hii imekuwa ikitumika katika ufundishaji kwa muda mrefu. Katika kujadiliana mwanafunzi mmoja mmoja hupata nafasi ya mawazo aliyonayo kuhusu suala linalojadiliwa na yeye pia huweza kupata mawazo yaw engine. Katika majadiliano mwanafunzi hupata ujuzi mpya nje na ule aliokuwa nao kabla hajashiriki kat...

DHANA YA MATUMIZI YA LUGHA, REJESTA, UTATA

Matumizi ya lugha ni namna ambavyo wazungumzaji wa lugha hutumia lugha kwa kuzingatia mila, desturi na kaida mbalimbali za jamii inayohusika. Katika mada hii utajifunza mambo ya msingi ya kuzingatia unapotumia lugha. Utaelewa dhana mbalimbali zinazohusishwa na matumizi ya lugha kama vile rejesta, misimu, utatata katika lugha, lugha ya mazungumzo na lugha ya maandishi. Matumizi ya lugha ni namna ambavyo wazungumzaji wa lugha hutumia lugha kwa kuzingatia mila, desturi na kaida mbalimbali za jamii inayohusika. Dhima ya matumizi ya lugha Dhima kuu ya lugha ni kupashana habari, ujuzi na maarifa mbalimbali. Vilevile lugha husaidia kujenga uhusiano mwema baina ya watu. Uhusiano huo unaweza kuwa wa kijamii, kielimu, kibiashara, kihuduma, kisiasa, kiuchumi n.k. Kwa hiyo, kujua jinsi ya kuitumia lugha kama inavyotakiwa, kunasaidia kufikisha vizuri ujumbe unaotakiwa bila kuupotosha. Vilevile kunasaidia kuepuka migongano, hasa ya kijamii kwa kuwa utakuwa umetumia lugha kwa mujibu wa mi...