Habarini marafiki,mlofunga hongereni, Nitakuwa mnafiki,nikijifanya sioni, Siyo ishara ya dhiki,bali mwongozo wa dini, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Wagonjwa na wengineo,mlioshindwa kufunga, Myafanye megineyo,itakavyo yenu funga, Sio kucheka wenzio,eti yule hakufunga, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Wewe usiye husika,naomba acha makwazo, Sije mtu kwazika,wewe ukawa ni chanzo, Mtu dini kaishika,kwako liwe kubwa funzo, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Na humu mitandaoni,si sehemu ya dhihaka, Eti nani simuoni,siyo lazima kwandika, Si mtafute simuni,siyo humu kuanika, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Pia ule unafiki,kujifanya umefunga, Waenda kwa marafiki,kuharibu yako funga, Mola hilo haafiki,ni bora usingefunga, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Liombeeni taifa,msisahau dunia, Tuyaepuka maafa,mola atawasikia, Pia wale walokufa,huko naijeria, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo.... |
Ushairi kama moja kati ya tanzu za fasihi inayowasilishwa katika namna zote aidha kwa lugha ya maandishi au kwa lugha ya masimulizi una mchango au nafasi kubwa sana katika kunufaisha au kustawisha maisha ya binadamu kwa kumuelimisha, kumsisimua, kutunza na kuhifadhi amali zake pamoja na kukuza na kuendeleza lugha yake kama moja kati ya vipengere muhimu maishani mwake. Ushairi kama nudhumu katika fasihi simulizi hujumuisha nyimbo, ngonjera, tenzi na mashairi yenyewe. Ushairi wa Kiswahili waweza kuainishwa katika tanzu au katika kumbo mbalimbli kama asemavyo Mulokozi (1996) kuwa zipo kumbo kuu tatu ambazo ni ushairi wa kijadi au kimapokeo, ushairi wa mlegezo au huru na ushairi wa maigizo. Wanazuoni wafuatao wa mashairi ya kimapokeo wametoa maana za ushairi kama ifuatavyo:- Shaaban Robert (1958:37). “Ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi. Zaidi ya kuwa na sanaa ya vina, ushairi una ufasaha wa maneno machache au muhtasari…, mawazo, maoni na fikra za ndani zi...
Comments
Post a Comment