Habarini marafiki,mlofunga hongereni, Nitakuwa mnafiki,nikijifanya sioni, Siyo ishara ya dhiki,bali mwongozo wa dini, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Wagonjwa na wengineo,mlioshindwa kufunga, Myafanye megineyo,itakavyo yenu funga, Sio kucheka wenzio,eti yule hakufunga, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Wewe usiye husika,naomba acha makwazo, Sije mtu kwazika,wewe ukawa ni chanzo, Mtu dini kaishika,kwako liwe kubwa funzo, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Na humu mitandaoni,si sehemu ya dhihaka, Eti nani simuoni,siyo lazima kwandika, Si mtafute simuni,siyo humu kuanika, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Pia ule unafiki,kujifanya umefunga, Waenda kwa marafiki,kuharibu yako funga, Mola hilo haafiki,ni bora usingefunga, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Liombeeni taifa,msisahau dunia, Tuyaepuka maafa,mola atawasikia, Pia wale walokufa,huko naijeria, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo.... |
Matumizi ya lugha ni namna ambavyo wazungumzaji wa lugha hutumia lugha kwa kuzingatia mila, desturi na kaida mbalimbali za jamii inayohusika. Katika mada hii utajifunza mambo ya msingi ya kuzingatia unapotumia lugha. Utaelewa dhana mbalimbali zinazohusishwa na matumizi ya lugha kama vile rejesta, misimu, utatata katika lugha, lugha ya mazungumzo na lugha ya maandishi. Matumizi ya lugha ni namna ambavyo wazungumzaji wa lugha hutumia lugha kwa kuzingatia mila, desturi na kaida mbalimbali za jamii inayohusika. Dhima ya matumizi ya lugha Dhima kuu ya lugha ni kupashana habari, ujuzi na maarifa mbalimbali. Vilevile lugha husaidia kujenga uhusiano mwema baina ya watu. Uhusiano huo unaweza kuwa wa kijamii, kielimu, kibiashara, kihuduma, kisiasa, kiuchumi n.k. Kwa hiyo, kujua jinsi ya kuitumia lugha kama inavyotakiwa, kunasaidia kufikisha vizuri ujumbe unaotakiwa bila kuupotosha. Vilevile kunasaidia kuepuka migongano, hasa ya kijamii kwa kuwa utakuwa umetumia lugha kwa mujibu wa mi...

Comments
Post a Comment