Posts

Showing posts from July, 2017

FUNGATE YA UHURU

Tuanze uhakiki huu, kwa kuanza na : KIPENGELE CHA MAUDHUI Dhamira Hili ni wazo kuu au mawazo mbalimbali yanayojitokeza katika kazi ya fasihi. Na katika diwani hii kuna dhamira kuu na dhamira ndogondogo ambazo zimejitokeza, kwa kuanza tunaanza na; Dhamira kuu Dhamira kuu ni wazo kuu linalojitokeza katika kazi za fasihi, na katika diwani hii, wazo kuu ni ukombozi wa jamii, sasa tuanzekuangalia ukombozi huo wa jamii, namna unavyojadiliwa katika diwani hii: Ukombozi wa jamii Dhamira kuu inayojitokeza katika diwani hii ni ukombozi wa jamii, mwandishi amejadili ukombozi huo katika Nyanja mbalimbali kama vile ukombozi wa kisiasa, kiuchumi na kiutamduni. Ukombozi wa kisiasa Kwa kiasi kikubwa mwandishi amejadili ukombozi wa kisiasa, mwandishi anaona kuwa ili jamii iweze kujikomboa kisiasa, jamii hiyo haina budi kuondokana na matatizo ya kiungozi [uongozi mbaya] uongozi ambao hauwajali wananchi zaidi ya kujali matumbo yao na maisha yao huku wakiwaacha wananchi waliowengi wakiishi maish

KILIO CHETU

TAHAKIKI TAMTHILIYA YA KILIO CHETU KIDATO CHA 3&4  JINA LA TAMTHILIYA: Kilio Chetu MWANDISHI: MEDICAL AID FOUNDATION MCHAPISHAJI: TANZANIA PUBLISHING HOUSE (TPH) MWAKA 1995 JINA LA MHAKIKI: Mwl. Furaha Venance Mawasiliano 0715 33 55 58 Mwaka 2014 UTANGULIZI Kilio Chetu ni tamthiliya inayojikita kuzungumzia umuhimu wa elimu ya jinsia na ukimwi kwa vijana, Tamthiliya hii inaonesha namna ukosefu wa elimu ya jinsia na ukimwi kwa jamii hususani vijana inavyochangia mimba za utotoni au mimba zisizotarajiwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa vijana. Katika tamthiliya hii, mwandishi anaonesha namna ambavyo jamii ikiangaika kujielimisha kuhusu elimu hii ya jinsia na ukimwa na kuwaacha vijana wakiangamia kwa kukosa elimu hiyo, hali hii inaifanya jamii kugawanyika, wapo wanaoona kuwa suluhisho la janga hili la Ukimwi, ni jamii nzima wakiwemo na vijana kupewa elimu hii lakini wapo wazazi wanaopinga wakiamini vijana umri wao wakupewa elimu hii haujafika bado. Je ni nini hatima y