Ushairi kama moja kati ya tanzu za fasihi inayowasilishwa katika namna zote aidha kwa lugha ya maandishi au kwa lugha ya masimulizi una mchango au nafasi kubwa sana katika kunufaisha au kustawisha maisha ya binadamu kwa kumuelimisha, kumsisimua, kutunza na kuhifadhi amali zake pamoja na kukuza na kuendeleza lugha yake kama moja kati ya vipengere muhimu maishani mwake.
Ushairi kama nudhumu katika fasihi simulizi hujumuisha nyimbo, ngonjera, tenzi na mashairi yenyewe. Ushairi wa Kiswahili waweza kuainishwa katika tanzu au katika kumbo mbalimbli kama asemavyo Mulokozi (1996) kuwa zipo kumbo kuu tatu ambazo ni ushairi wa kijadi au kimapokeo, ushairi wa mlegezo au huru na ushairi wa maigizo.
Wanazuoni wafuatao wa mashairi ya kimapokeo wametoa maana za ushairi kama ifuatavyo:-
Shaaban Robert (1958:37).
“Ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi. Zaidi ya kuwa na sanaa ya vina, ushairi una ufasaha wa maneno machache au muhtasari…, mawazo, maoni na fikra za ndani zinazoelezwa kwa muhtasari wa ushairi huvuta moyo kwa namna ya ajabu”.
Mathias Mnyampala (1965:Dibaji)
“ushairi ni msingi wa maneno ya hekima tangu kale, ndicho kitu kilicho bora sana katika maongozi ya dunia kwa kutumia maneno ya mkato na lugha nzito yenye kunata iliyopangwa kwa urari wa vina na mizani maalumu kwa shairi”.
Amri Abedi (1954:1).
“Ushairi au utenzi ni wimbo, hivyo kama shairi haliimbiki, halina maana”.
Mbali na maana hizo za ushairi kwa mujibu wa wanamapokeo, zifuatazo ni maana za ushairi kwa mujibu wa wanamlegezo:-
Kezilahabi katika mbonde, J.M (1976:123).
Ushairi ni tukio, hali au wazo ambalo limeoneshwa kwetu kutokana na upangaji mzuri wa maneno fasaha yenye mizani kwa kifupi ili kuonesha ukweli fulani wa maisha.
Topani (1974:X).
“Anasema, shairi ni utungo unaoeleza hisia za undani za binadamu kwa mpangilio fulani wa maneno”.
Mlokozi na Kahigi (1982:25).
Wao wanatafsiri ushairi kuwa ni sanaa ilyopambanuliwa kwa mpangilio maalumu wa maneno fasaha na yenye muwala, kwa lugha ya mkato, picha, sitiari au ishara, katika usemi, maandishi au mahadhi ya wimbo, ili kuleta wazo au mawazo, kufunza au kueleza tukio au hisia fulani kuhusu maisha au mazingira ya binadamu kwa njia inayogusa moyo.
Kwa ujumla na kwa kawaida fasiri ya ushairi ilyozoeleka bila kujali ni wa kimapokeo au mlegezo, ni ile isemayo kuwa ushairi ni sanaa inayotumia lugha teule na mpangilio fulani wa maneno ili kuweza kufikisha ujumbe lengwa kwa jamii. Ushairi ni tofauti na nathari kwani hauelezi tu bali huonesha hisi, wazo, hali kitu au tukio fulani kwa kuathiri hisia zetu. Na kuhusu kuwepo kwa makundi ya wanamapokeo na wanamlegezo au wanamapinduzi ni kutokana na imani zao kuhusu ushairi. Wanamapokeo ni wale washairi wa jadi wanaoshikilia kuwa ili utungo fulani uweze kuwa shairi ni lazima utungo huo ufuate sheria na kanuni fulani kama vile ulali wa vina na mizani, idadi, idadi maalumu ya mishororo katika beti ambazo huitwa arudhi, na wanamlegezo/wanamapinduzi/wanausasa ni wale wanao amini kuwa ili utungo Fulani uweze kuingia katika kundi la mashairi si lazima uzingatie arudhi.Kundi hili husisitiza kuwa la muhimu katika utungo nsiyo sheria bali ni ujumbe au maudhui/malengo kwa hadhira yake.
Kutokana na mitazamo inayotumiwa na wanamapokeo na wanausasa katika kutafsiri ushairi, inaonesha kuwa tafsiri zao zinalingana katika namna/vipengele vifuatavyo;
Ushairi ni wimbo. Wataalamu wa pande zote mbili wanaamini kuwa kitu kinachoitwa ushairi ni sharti kiwe katika mahadhi ya wimbo ,yaani kiweze kuimbika. Mfano, Mwanamapokeo Amri
Abeid(1954:1) anasema ushairi ni wimbo, hivyo basi shairi kama haliimbiki halina maana.Wakati mwana mapinduzi Mulokozi nae anasema lazima shairi liwe na mahadhi ya wimbo(liimbike)
Ushairi ni sanaa; Wanamapokeo na wanamapinduzi katika kueleza maana ya ushairi wanaamini kuwa ushairi ni kazi ya sanaa. Hii inamaana kwamba kuna ufundi maalumu unaotumika kusuka/kutunga mashairi. Hii inaweza kuthibitishwa na mwanamapokeo Shaaban Robert na mwanamlegezo Mlokozi na Kaligi ambao wote wanaelezea ushairi kuwa ni sanaa.
Ushairi unailenga na kuibua hisia za jamii.Wanazuoni wa pande zote mbili wa kimapokeo na wa kisasa wanaamini kuwa ushairi ni lazima ulenge na kuibua hisia za jamii.Kwa mfano wanamapokeo Mathuis Mnyampala (1965) na Shaban Robeert (1958) pia wanamapinduzi na Kahigi(1982) pamoja na Topan (1974) wote wanasisitiza kuwa ushairi ni lazima uilenge jamii kwa kuibua hisia za jamii hiyo husika.
Ushairi hutumia lugha (maneno) ambayo ni fasaha.Jambo hili katika ushahiri linatiliwa mkazo na wanazuon i wa makundi yote .Mfano wale wa kimapokeo na hata wa kisasa.Wataalamu waoweza kuthibitishia hili ni mwanamapinduzi Kazilahabi ambaye anasema ushahiri huwa na uzuri wa maneno fasaha na mwanautamaduni Shaban Robert asemaye kuwa ushairi huwa na ufasaha wa maneno.
Pamoja na ulinganifu huo unaojitokeza baina ya wataalamu wa mashairi ya kimapokeo na wale wa mashairi ya kimlegezo katika kutoa maana ya ushairi, bado kuna migongano kadha wa kadha ya kimtazamo inayo wafanya wahitilafiane. Tofauti zao ni pamoja na hizi zifuatazo;
Urari wa vina na mizani (arudhia). Wanamashairi karibuni wote wa kimapokeo wanasisitiza kuwa utungo ili uitwe shairi lazima taratibu maalumu za utunzi kama anavyoeleza mathius Mnyampala (1965) ufanano(urari ) wa vina na mizani. Lakini wana ushairi wa kimapinduzi wote hawaoni umuhimu wa jambo hilo, wao wanaona utungo uwao wowote ule unaweza kuwa shairi ilimradi ufikishe ujumbe kwa jamii. Kwa wanamapinduzi kuhusu urari wa vina na mizani ni kazi ya ziada isiyo ya lazima katika mashairi.
Idadi ya mistari, wana ushairi wa kimapokeo wanasisitiza kuwa katika usahairi lazima kuwa na idadi maalumu ya mishororo katika kila ubeti na ni shariti iadadi hiyo ifanane kwa beti zote lakini wataalamu wa mashairi ya kisasa wao wanaona shairi hata ukiwa na idadi ya mistari inayotofautiana katika beti zote ni sawa tu, cha kuzingatia ni maudhui yaliyomo na sio fani.
Ni maneno ya hekima tangu kale, kama asemavyo mwanamapokeo Mathias Mnyapala (1965:Dibaji) lakini mashairi ya kimlegezo ni mpya yameibuka baada ya mashairi ya kimapokeo. Kwa wanamashairi wa kisasa wanaamini kuwa umri sio kigezo cha kufafanulia mashairi na huweza kutumia lugha yeyote aipendayo mtunzi
Matumizi ya lugha, mashairi kwa mujibu wa wanamapokeo lazima yatumie lugha ya mkato na mnato lakini wanamapinduzi wanaona hicho si kigezo cha msingi katika utoajiwa maana ya ushairi ,mshairi atumie lugha kadri awezavyo yeye. Mfano Mathias Mnyapala na Shabani Robert (Wanamapokeo) wanasisitiza matumizi ya lugha ya mnato na mkato lakini wanamapinduzihawaongelei suala hili katika kutoa maana ya mashairi au ushairi.
Pamoja na ufanano au ulinganifu na utofauti unaojitokeza baina ya wanzuoni wa kisasa na wale wa kimapokeokatika kueleza au kutoa maana ya mashairi pia ni vyema kuwa ushairi uzingatie mambo yafuatayo;
Ni vyema ushairi ubadilike kutokana na wakati na mazingira, mashairi lazima yapambanue matukio halisi yanayotokea katika jamii husika na katika wakati huo. Mfano, katika kipindi cha mafuriko basi washairi watunge mashairi yanohusu mafuriko kwa ajili ya jamii hiyo iliyokumbwa na janga hilo, jamii nyingine itakayokubwa na janga la njaa basi ushairi wao uwe ni wa kuhusu suala hilo katika kipindi hicho.
Aidha pamoja na kuwepo kwa watu wenye vipawa vya ushairi kwa kuzaliwa navyo, haina budi pia kutumia wataalamu waliosomea maishairi katika kutoa fasili za ushairi na kutengeneza diwani za mashairi badala ya kuwa kila mtu anazungumza anachofikiri yeye kuhusu ushairi na mashairi
Kwa ujumla mashairi yoyote yale, yawe ya kimapokeo au ya kisasa ni mashairi tu ili mradi jamii inufaike kutokana na mashairi hayo kwa kusisimka, kuelimika, kutunziwa amali zake na kukuziwa na kuendelezewa lugha yake.
MAREJEO.
Abeid, A. (1954). Sheria za kutunga Mashairi na Diwani ya AMR. EALB, Nairobi.
Mulokozi,M.M. na Kahigi.K.K(1982). Kutunga za Ushairi na Diwani Yetu. TPH, Dar es salaam.
Robert,S.(1958). Hotuba juu ya Ushairi. JeASC 28/1:37-42.
Mnyampala, M. (1965). Diwani ya Mnyamlepa, EALB, Nairobi.
Topan F (1974). “Dibaji” katika Kezilahabi ukurasa:x.
Kezilahabi, E. (1976). Ushairi wa mapokeo na wa wakati ujao. Katika Mbonde J.P. 121-137
Ushairi kama nudhumu katika fasihi simulizi hujumuisha nyimbo, ngonjera, tenzi na mashairi yenyewe. Ushairi wa Kiswahili waweza kuainishwa katika tanzu au katika kumbo mbalimbli kama asemavyo Mulokozi (1996) kuwa zipo kumbo kuu tatu ambazo ni ushairi wa kijadi au kimapokeo, ushairi wa mlegezo au huru na ushairi wa maigizo.
Wanazuoni wafuatao wa mashairi ya kimapokeo wametoa maana za ushairi kama ifuatavyo:-
Shaaban Robert (1958:37).
“Ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi. Zaidi ya kuwa na sanaa ya vina, ushairi una ufasaha wa maneno machache au muhtasari…, mawazo, maoni na fikra za ndani zinazoelezwa kwa muhtasari wa ushairi huvuta moyo kwa namna ya ajabu”.
Mathias Mnyampala (1965:Dibaji)
“ushairi ni msingi wa maneno ya hekima tangu kale, ndicho kitu kilicho bora sana katika maongozi ya dunia kwa kutumia maneno ya mkato na lugha nzito yenye kunata iliyopangwa kwa urari wa vina na mizani maalumu kwa shairi”.
Amri Abedi (1954:1).
“Ushairi au utenzi ni wimbo, hivyo kama shairi haliimbiki, halina maana”.
Mbali na maana hizo za ushairi kwa mujibu wa wanamapokeo, zifuatazo ni maana za ushairi kwa mujibu wa wanamlegezo:-
Kezilahabi katika mbonde, J.M (1976:123).
Ushairi ni tukio, hali au wazo ambalo limeoneshwa kwetu kutokana na upangaji mzuri wa maneno fasaha yenye mizani kwa kifupi ili kuonesha ukweli fulani wa maisha.
Topani (1974:X).
“Anasema, shairi ni utungo unaoeleza hisia za undani za binadamu kwa mpangilio fulani wa maneno”.
Mlokozi na Kahigi (1982:25).
Wao wanatafsiri ushairi kuwa ni sanaa ilyopambanuliwa kwa mpangilio maalumu wa maneno fasaha na yenye muwala, kwa lugha ya mkato, picha, sitiari au ishara, katika usemi, maandishi au mahadhi ya wimbo, ili kuleta wazo au mawazo, kufunza au kueleza tukio au hisia fulani kuhusu maisha au mazingira ya binadamu kwa njia inayogusa moyo.
Kwa ujumla na kwa kawaida fasiri ya ushairi ilyozoeleka bila kujali ni wa kimapokeo au mlegezo, ni ile isemayo kuwa ushairi ni sanaa inayotumia lugha teule na mpangilio fulani wa maneno ili kuweza kufikisha ujumbe lengwa kwa jamii. Ushairi ni tofauti na nathari kwani hauelezi tu bali huonesha hisi, wazo, hali kitu au tukio fulani kwa kuathiri hisia zetu. Na kuhusu kuwepo kwa makundi ya wanamapokeo na wanamlegezo au wanamapinduzi ni kutokana na imani zao kuhusu ushairi. Wanamapokeo ni wale washairi wa jadi wanaoshikilia kuwa ili utungo fulani uweze kuwa shairi ni lazima utungo huo ufuate sheria na kanuni fulani kama vile ulali wa vina na mizani, idadi, idadi maalumu ya mishororo katika beti ambazo huitwa arudhi, na wanamlegezo/wanamapinduzi/wanausasa ni wale wanao amini kuwa ili utungo Fulani uweze kuingia katika kundi la mashairi si lazima uzingatie arudhi.Kundi hili husisitiza kuwa la muhimu katika utungo nsiyo sheria bali ni ujumbe au maudhui/malengo kwa hadhira yake.
Kutokana na mitazamo inayotumiwa na wanamapokeo na wanausasa katika kutafsiri ushairi, inaonesha kuwa tafsiri zao zinalingana katika namna/vipengele vifuatavyo;
Ushairi ni wimbo. Wataalamu wa pande zote mbili wanaamini kuwa kitu kinachoitwa ushairi ni sharti kiwe katika mahadhi ya wimbo ,yaani kiweze kuimbika. Mfano, Mwanamapokeo Amri
Abeid(1954:1) anasema ushairi ni wimbo, hivyo basi shairi kama haliimbiki halina maana.Wakati mwana mapinduzi Mulokozi nae anasema lazima shairi liwe na mahadhi ya wimbo(liimbike)
Ushairi ni sanaa; Wanamapokeo na wanamapinduzi katika kueleza maana ya ushairi wanaamini kuwa ushairi ni kazi ya sanaa. Hii inamaana kwamba kuna ufundi maalumu unaotumika kusuka/kutunga mashairi. Hii inaweza kuthibitishwa na mwanamapokeo Shaaban Robert na mwanamlegezo Mlokozi na Kaligi ambao wote wanaelezea ushairi kuwa ni sanaa.
Ushairi unailenga na kuibua hisia za jamii.Wanazuoni wa pande zote mbili wa kimapokeo na wa kisasa wanaamini kuwa ushairi ni lazima ulenge na kuibua hisia za jamii.Kwa mfano wanamapokeo Mathuis Mnyampala (1965) na Shaban Robeert (1958) pia wanamapinduzi na Kahigi(1982) pamoja na Topan (1974) wote wanasisitiza kuwa ushairi ni lazima uilenge jamii kwa kuibua hisia za jamii hiyo husika.
Ushairi hutumia lugha (maneno) ambayo ni fasaha.Jambo hili katika ushahiri linatiliwa mkazo na wanazuon i wa makundi yote .Mfano wale wa kimapokeo na hata wa kisasa.Wataalamu waoweza kuthibitishia hili ni mwanamapinduzi Kazilahabi ambaye anasema ushahiri huwa na uzuri wa maneno fasaha na mwanautamaduni Shaban Robert asemaye kuwa ushairi huwa na ufasaha wa maneno.
Pamoja na ulinganifu huo unaojitokeza baina ya wataalamu wa mashairi ya kimapokeo na wale wa mashairi ya kimlegezo katika kutoa maana ya ushairi, bado kuna migongano kadha wa kadha ya kimtazamo inayo wafanya wahitilafiane. Tofauti zao ni pamoja na hizi zifuatazo;
Urari wa vina na mizani (arudhia). Wanamashairi karibuni wote wa kimapokeo wanasisitiza kuwa utungo ili uitwe shairi lazima taratibu maalumu za utunzi kama anavyoeleza mathius Mnyampala (1965) ufanano(urari ) wa vina na mizani. Lakini wana ushairi wa kimapinduzi wote hawaoni umuhimu wa jambo hilo, wao wanaona utungo uwao wowote ule unaweza kuwa shairi ilimradi ufikishe ujumbe kwa jamii. Kwa wanamapinduzi kuhusu urari wa vina na mizani ni kazi ya ziada isiyo ya lazima katika mashairi.
Idadi ya mistari, wana ushairi wa kimapokeo wanasisitiza kuwa katika usahairi lazima kuwa na idadi maalumu ya mishororo katika kila ubeti na ni shariti iadadi hiyo ifanane kwa beti zote lakini wataalamu wa mashairi ya kisasa wao wanaona shairi hata ukiwa na idadi ya mistari inayotofautiana katika beti zote ni sawa tu, cha kuzingatia ni maudhui yaliyomo na sio fani.
Ni maneno ya hekima tangu kale, kama asemavyo mwanamapokeo Mathias Mnyapala (1965:Dibaji) lakini mashairi ya kimlegezo ni mpya yameibuka baada ya mashairi ya kimapokeo. Kwa wanamashairi wa kisasa wanaamini kuwa umri sio kigezo cha kufafanulia mashairi na huweza kutumia lugha yeyote aipendayo mtunzi
Matumizi ya lugha, mashairi kwa mujibu wa wanamapokeo lazima yatumie lugha ya mkato na mnato lakini wanamapinduzi wanaona hicho si kigezo cha msingi katika utoajiwa maana ya ushairi ,mshairi atumie lugha kadri awezavyo yeye. Mfano Mathias Mnyapala na Shabani Robert (Wanamapokeo) wanasisitiza matumizi ya lugha ya mnato na mkato lakini wanamapinduzihawaongelei suala hili katika kutoa maana ya mashairi au ushairi.
Pamoja na ufanano au ulinganifu na utofauti unaojitokeza baina ya wanzuoni wa kisasa na wale wa kimapokeokatika kueleza au kutoa maana ya mashairi pia ni vyema kuwa ushairi uzingatie mambo yafuatayo;
Ni vyema ushairi ubadilike kutokana na wakati na mazingira, mashairi lazima yapambanue matukio halisi yanayotokea katika jamii husika na katika wakati huo. Mfano, katika kipindi cha mafuriko basi washairi watunge mashairi yanohusu mafuriko kwa ajili ya jamii hiyo iliyokumbwa na janga hilo, jamii nyingine itakayokubwa na janga la njaa basi ushairi wao uwe ni wa kuhusu suala hilo katika kipindi hicho.
Aidha pamoja na kuwepo kwa watu wenye vipawa vya ushairi kwa kuzaliwa navyo, haina budi pia kutumia wataalamu waliosomea maishairi katika kutoa fasili za ushairi na kutengeneza diwani za mashairi badala ya kuwa kila mtu anazungumza anachofikiri yeye kuhusu ushairi na mashairi
Kwa ujumla mashairi yoyote yale, yawe ya kimapokeo au ya kisasa ni mashairi tu ili mradi jamii inufaike kutokana na mashairi hayo kwa kusisimka, kuelimika, kutunziwa amali zake na kukuziwa na kuendelezewa lugha yake.
MAREJEO.
Abeid, A. (1954). Sheria za kutunga Mashairi na Diwani ya AMR. EALB, Nairobi.
Mulokozi,M.M. na Kahigi.K.K(1982). Kutunga za Ushairi na Diwani Yetu. TPH, Dar es salaam.
Robert,S.(1958). Hotuba juu ya Ushairi. JeASC 28/1:37-42.
Mnyampala, M. (1965). Diwani ya Mnyamlepa, EALB, Nairobi.
Topan F (1974). “Dibaji” katika Kezilahabi ukurasa:x.
Kezilahabi, E. (1976). Ushairi wa mapokeo na wa wakati ujao. Katika Mbonde J.P. 121-137
Kazi mzuri sana...
ReplyDeleteKazi nzuri hii ajabu
ReplyDeleteKazi nzuri. Ubarikiwe
ReplyDeleteMashiri ibarikiwe
ReplyDeleteMashiri ibarikiwe
ReplyDeleteKazi safi
ReplyDeleteUshairi ni utungo wa kimasikizi unaotumia lugha ya mjazo ipi kufikisha ujumbe kwa jamii.
ReplyDeleteUshairi, Ni sanaa ya lugha ya mkato yenye ubunifu unaoelezea jambo kwa kuvutia hisia
ReplyDeleteShukrani kabisa
ReplyDeleteUshairi ni tungo inayo zingatia urari wa vina na mizani ...nalengo lake kufikisha ujumbe kwa hadhira kusudiwa
ReplyDeleteKazi nzuri sana nimesoma nimeelewa vizuri
ReplyDelete