Skip to main content

tofauti ya kiisimu na kilahaja katika matumizi ya lugha



SWALI.
Kwa kutumia mifano kutoka katika lugha za makabila ya Tanzania, onyesha utofauti wa kiisimu na kilahaja katika matumizi ya lugha.             



Lugha ni mpangilio wa sauti na maneno unaoleta maana ambao hutumiwa na watu wa taifa au kundi fulani kwa ajili ya mawasiliano. Lugha ni maneno pamoja na matumizi yake. (TUKI 2013).
Lugha; ni mfumo wa sauti za nasibu zilizokua katika mpango maalumu na zilizokubaliwa na jamii ya watu fulani ili zitumike katika mawasiliano.
Lahaja ni tofauti katika matamshi, maumbo, na matumizi ya maneno katika maeneo mbalimbali kwa lugha yenye asili moja. (TUKI, 2013).
Lahaja ni vijilugha vinavyoibuka kwa lugha moja kuu kutokana na tofauti za kijiografia, kitabaka baina ya wazungumzaji wa lugha hiyo. Watu hao hutofautiana kimatamshi, muundo wa sentensi au msamiati.
Zifuatazo ni tofauti za kiisimu kutoka katika makabila ya Tanzania katika matumizi ya lugha:-
Lafudhi, hii ni tofauti mojawapo katika tofauti zinazojitokeza kwenye makabila ya Tanzania. Ile hali ya upekee wa mtu katika matamshi unaoathiriwa na lugha mama, mazingira yake ya kijiografia au ujuzi wake wa lugha inapelekea kutokea kwa utofauti. Mfano wasukuma lafudhi yao imejikita katika ukazaji wa maneno, kwa mfano neno ntakupiga silabi pi hutamkwa kwa mkazo wa hali ya juu.
Kiimbo, ule upandaji na ushukaji wa sauti katika utamkaji wa maneno hutofautia katika kila lugha na kila kabila. Mfano mnyakyusa anaposema ugonile herufi u hutamkwa kwa sauti ya juu ambapo maneno mengine hutamkwa kwa kushusha sauti. Wakati huohuo wasukuma wanaposema mwangaluka neno mwa na ka hutamkwa kwa sauti ya juu kuliko maneno ya kati. Hivyo kuna utofauti mkubwa sana wa kiimbo katika makabila ya Tanzania.
Mkazo, katika mkazo wa baadhi ya maneno katika utamkaji, makabila mbalimbali yanatamka kwa mtindo tofautitofauti. Kwa mfano kabila kama wakurya neno ninkutema neno te hutamkwa kwa mkazo sana kuliko maneno mengine. Lakini pia wanyakyusa utamkaji wao ni tofauti kidogo, kwa mfano neno ninkukoma neno ko hutamkwa kwa mkazo kuliko maneno mengine. Hivyo kuna utofauti mkubwa sana wa kiisimu katika makabila ya Tanzania.
Toni, makabila mbalimbali hutofautiana katika toni ambapo kila kabila lina toni yake katika utamkaji wa maneno. Kile kiwango fulani cha juu au cha chini cha sauti ndicho kinachotofautisha, mfano kabila la wahaya toni yao huwa ni ya chini ukilinganisha na toni ya wasukuma ambayo huwa ni ya juu. Wahaya katika neno zebilo(za siku) huwa na toni ya chini, wakati wasukuma neno jamashiku(za siku) huwa na toni ya juu. Hivyo kuna utofauti mkubwa wa kiisimu katika makabila ya Tanzania.
Utamkaji wa maneno, pia katika utamkaji wa maneno kuna utofauti mkubwa sana kutokana na makabila. Kwa mfano kabila la wahaya neno ng’ombe wenyewe husema ngombe, lakini pia wakurya wametawaliwa sana na matumizi ya r, kwa mfano neno kula ambacho ni kitendo wenyewe husema au hutamka kura. Hivyo kuna utofauti mkubwa sana wa utamkaji wa maneno katika makabila ya Tanzania.
Msamiati, kila lugha ina utaratibu wake wa kujisimamia katika msamiati. Hii hupelekea kutofautiana kwa misamiati katika makabila hapa Tanzania. Kwa mfano neno makande hutamkwa kwa misamiati tofautitofauti kutokana na kabila lenyewe. Wasukuma husema masangu lakini wanyakyusa husema ingati, hivyo kuna utofauti mkubwa sana kimsamiati.
Baada ya kuangalia tofauti za matumizi ya lugha kiisimu, ngoja tuone tofauti za kilahaja katika matumizi ya lugha. Hapa nitajikita zaidi katika kabila la wahaya na kabila la wazinza ambao wametenganishwa na ziwa Victoria:-
Msamiati, katika msamiati wazinza na wahaya hutofautiana sana. Katika Kiswahili kuna maji, wazinza husema amenzi na wahaya husema amaizi. Pia neno kesho wazinza husema nyencha wakati wahaya husema nyenkya Hivyo katika msamiati kuna utofauti wa kilahaja kati ya wazinza na wahaya kwani kuna vijitofauti vidogovidogo vinavyojitokeza katika maneno yaani msamiati.
Sentensi, kuna tofauti ya kilahaja katika sentensi za kizinza na zile za kihaya.
Kwa mfano katika Kiswahili: mama amelala
                             Kihaya:  mai yanyamile.
                             Kizinza: maa yalyamile
Hapo tunaona katika sentensi kuna tofauti ndogondogo zinazojitokeza, mpangilio wa maneno upo sawa lakini tofauti ipo kwenye nomino mai kwa wahaya na maa kwa wazinza. Na katika kitenzi yanyamile kwa wahaya, na yalyamile kwa wazinza.
Mofolojia, katika hii taaluma inayohusika na maumbo wazinza na wahaya hutofautiana kwa kiasi kidogo sana.
                      Kwa mfano: Kiswahili-anasoma
                                         Kihaya- nashoma
                                         Kizinza- nasoma
Kwa kuangalia mifano hiyo tunaweza kuona kwamba katika kutenganisha viambishi hufuata kanuni moja, kwa mfano kinapokaa kiambishi cha njeo kwenye kihaya ndipo pia hukaa katika kizinza isipokua hutofautiana katika mzizi. Kihaya mzizi ni shom na kizinza mzizi ni som.
Matamshi, katika matamshi wahaya hutamka maneno ya mwanzo kwa juu na kumalizia kwa kushusha sauti wakati wazinza hutamka kwa sauti iliyo lala.
                         Kwa mfano Kiswahili- jembe
                                            Kihaya- enfuka
                                            Kizinza- enfuka
Neno “e” kwa wahaya hutamka kwa juu sana na kumalizia maneno mengine kwa sauti ya chini sana, wakati wazinza hutamka kwa sauti ya kulala.
Kiujumla kila lugha inatofautiana na lugha nyingine katika Nyanja mbalimbali zikiwemo matamshi, maumbo, msamiati na maana ya maneno. Hivyo ni vizuri kwa kila watumiaji wa lugha(makabila) watumie lugha kutokana na eneo wanaloishi kwani kuna baadhi ya maneno yakitumiwa katika mazingira mengine hubadili maana.




MAREJELEO
Msanjila, Kihole, Massamba(2011): IsimuJamii Sekondari Na Vyuo. TUKI, UDSM.
TUKI (2013): Kamusi ya Kiswahili sanifu. Chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Comments

Popular posts from this blog

KISWAHILI FORM 1: FASIHI SIMULIZI

KISWAHILI Form 1 Topic 4 FASIHI SIMULIZI Fasihi simulizi ni moja kati ya tanzu za fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo. Katika mada hii utajifunza na kisha utaweza kubainisha tanzu na vipera vya fasihi simulizi pamoja na ufafanuzi wake. Na pia utaweza kutofautisha kati ya kipera na kipera au kati ya utanzu na utanzu. Ubainishaji wa Tanzu za Fasihi Simulizi Tanzu za Fasihi Simulizi Bainisha tanzu za fasihi simulizi Fasihi Simulizi ni kazi ya fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo kama vile; hadithi, ngoma na vitendawili. Tanzu za Fasihi Simulizi ni pamoja na hizi zifuatazo: Masimulizi/hadithi Semi Ushairi Mazungumzo Maigizo Ngomezi Ufafanuzi wa Vipera vya Tanzu za Fasihi Simulizi Vipera vya Hadithi Fafanua vipera vya hadithi SIMULIZI/ HADITHI Masimulizi ni fasihi yenye kusimulia habari fulan...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

Mbinu za kufundishia , ni miongozo mbalimbali atumiayo mwalimu wakati wa kufundisha somo aliloliandaa kwa wanafunzi wake. Walimu wanapaswa kuamua kwa kuchagua kwa makini njia na mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Ziko njia nyingi za kutengeneza mazingira ya mtoto aweze kujifunza na pia ziko mbinu nyingi za kufundishia. Pamoja na wingi huo tunaweza kuzigawa katika makundi makuu mawili kadri ya jinsi zinavyowashirikisha watoto katika tendo la kujifunza, ambazo tunaweza kuziita shirikishi na zisizo shirikishi . Zifuatazo ni baadhi ya mbinu shirikishi na zisizo shirikishi za kufundishia pamoja na faida na hasara zake:- Njia ya majadiliano , njia hii imekuwa ikitumika katika ufundishaji kwa muda mrefu. Katika kujadiliana mwanafunzi mmoja mmoja hupata nafasi ya mawazo aliyonayo kuhusu suala linalojadiliwa na yeye pia huweza kupata mawazo yaw engine. Katika majadiliano mwanafunzi hupata ujuzi mpya nje na ule aliokuwa nao kabla hajashiriki kat...

DHANA YA USHAIRI ILIVYOFAFANULIWA NA WATAALAMU MBALIMBALI

Ushairi kama moja kati ya tanzu za fasihi inayowasilishwa katika namna zote aidha kwa lugha ya maandishi au kwa lugha ya masimulizi una mchango au nafasi kubwa sana katika kunufaisha au kustawisha maisha ya binadamu kwa kumuelimisha, kumsisimua, kutunza na kuhifadhi amali zake pamoja na kukuza na kuendeleza lugha yake kama moja kati ya vipengere muhimu maishani mwake. Ushairi kama nudhumu katika fasihi simulizi hujumuisha nyimbo, ngonjera, tenzi na mashairi yenyewe. Ushairi wa Kiswahili waweza kuainishwa katika tanzu au katika kumbo mbalimbli kama asemavyo Mulokozi (1996) kuwa zipo kumbo kuu tatu ambazo ni ushairi wa kijadi au kimapokeo, ushairi wa mlegezo au huru na ushairi wa maigizo. Wanazuoni wafuatao wa mashairi ya kimapokeo wametoa maana za ushairi kama ifuatavyo:- Shaaban Robert (1958:37). “Ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi. Zaidi ya kuwa na sanaa ya vina, ushairi una ufasaha wa maneno machache au muhtasari…, mawazo, maoni na fikra za ndani zi...