- MAANA YA FASIH NA UCHAMBUZI WA VIPERA
- MAANA NA METHALI ZILIZOKUSANYWA
- FILAMU NI SEHEMU YA FASIHI YA KISWAHILI
MAANA YA FASIHI NA UCHAMBUZI WA VIPERA VYAKE
Williady, (2015) Fasihi ni tawi moja wapo la sanaa linalotumia lugha katika kuwasilisha ujumbe wa mdomo au wa maandishi.
Wamitila (2004) Fasihi ni sanaa inayotumia luha na ambayo hujishughulisha na binadamu pamoja na maisha yake na huathri, hugusa au huacha athari fulanina hupatikana katika umbo ambalo linatambuliwa na jamii Fulani.
Kwakuwa fasihi ni aina ya sanaa, ni vyema mwanafunzi akajua pia maana ya sanaa.
MAANA YA SANAA
(Williady: 2015) Sanaa ni ujuzi au ufundi wenye kuleta manufaa kwa uma.
UMBO LA SANAA
Tunaposema umbo la sanaa tunamaanisha matawi yanayojenga sanaa. Matawi hayo nipamoja na;
Fasihi, maonyesho, ususi, uhunzi, ufumaji, utarizi, uchongaji, ufinyanzi, uchoraji na muziki.
AINA/ KUMBO/ TANZU ZA FASIHI
Katika kumbo ya fasihi na taaluma zake kuna aina kuu mbili za fasihi, ambazo ni;
Fasihi Simulizi
Fasihi Andishi
TOFAUTI KATI YA FASIHI SIMULIZI NA FASIHI ANDISHI
Namna ya uwasilishaji wake. Fasihi simulizi huwasilishwa kwa njia yam domo wakati fasihi andishi uwasilishwa kwa njia ya maandishi.
Mabadiliko. Fasihi simulizi huweza kupokea mabadiliko ya papo kwa papo wakati fasihi andishi hurekebishwa baada ya toleo jipya.
Utendaji wake kwa hadhira na fanani. Hadhira na fanani katika fasihi simulizi huwa ni yakiutendaji, wasikilizaji wanaweza kuchangia mawazo kwa kutoa maoni, kuuliza maswali au kushadadia masimulizi ya fanani. Fasihi andishi hadhira hawawezi kuchangia lolote.
Ukongwe. Fasihi simulizi niyazamani zaidi, ilianza wakati mwanadamu alipoanza kutumia mdomo katika mawasiliano. Fasihi andishi ilianza pindi maandishi yalipobuniwa.
Vidato na elimu. Fasihi simulizi haiitaji mtu ajue kusoma ama kuandika, inamuhitaji mtu mwenye uwezo wa kuzungumza. Fasihi andishi inamhitaji mtu anayejua kuandika na kusoma.
Umiliki. Fasihi simulizi inamilikiwa na jamii nzima wakati fasihi andishi humilikiwa na mwandishi aliyeandika na kupiga chapa kazi hiyo.
Idadi ya tanzu. Fasihi simulizi inatanzu nyingi zaidi kuliko fasihi andishi.
Kuhifadhi. Hapo kale fasihi simulizi ilihifadhiwa kichwani, kwa sasa fasihi simulizi yaweza kuhifadhiwa katika vinasa sauti, kaseti na santuri. Fasihi andishi yenyewe huifadhi wake ni kwa njia ya maandishi.
Mwingiliano wa tanzu kwa kiasi. Fasihi simulizi huweza kuingiliwa kwa kiasi kikubwa na tanzu nzingine kama vile methali, vitendawili, nyimbo na nahau wakati fasihi andishi huweza kuingiliwa na tanzu nyingine kwa kiasi kidogo.
UFAFANUZI WA AINA ZA FASIHI
1.Fasihi simulizi
Fasihi simulizi ni aina ya fasihi inayotumia mdomo na utendaji wa viungo vya mwili katika kuwasilisha maudhui ya fanani kwa hadhira iliyokusudiwa.
TANZU ZA FASIHI SIMULIZI
Hadithi, uigizaji, ushairi na semi
VIPERA VYA HADIDHI
Ngano, vigano, hekaya, soga, tarihi, visa, visasili, shajara, istiala, michapo na mbazi
VIPERA VYA UIGIZAJI
Miviga, michezo ya jukwaani, majigambo, utani, vichekesho, ngonjera, mgomezi na
mazungumzo
mazungumzo
VIPERA VYA USHAIRI
Nyimbo, maghani, ngonjera, mashairi, tenzi na tendi
AINA ZA NYIMBO
Bembezi, nyimbo za mapenzi, nyiso, nyimbo za jadi, nyimbo za harusi, nyimbo za watoto
nyimbo za sifa, nyimbo za kampeni, nyimbo za maombolezo na nyimbo za chombezi.
nyimbo za sifa, nyimbo za kampeni, nyimbo za maombolezo na nyimbo za chombezi.
VIPERA VYA SEMI
Methali, misimu, lakabu, nahau, vitendawili. utani, misimu, mafumbo, masaguo, mizungu na
misemo
misemo
MAJUKUMU / DHIMA ZA FASIHI SIMULIZI KATIKA JAMII
Kuelimisha, kuburudisha, kusisimua, ukombozi, kutoa mwongozo kwa jamii, kutunza amali
za jamii (historia na utamaduni), kujuza na kuunganisha vizazi nz vizazi, kufundisha,
kudumisha uhusiano, kudumisha ushirikiano na kukuza stadi za lugha
za jamii (historia na utamaduni), kujuza na kuunganisha vizazi nz vizazi, kufundisha,
kudumisha uhusiano, kudumisha ushirikiano na kukuza stadi za lugha
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA USIMULIZI WA HADITHI
Ili msimuliaji aweze kutongoa au kusimulia hadithi kwa usahihi inampasa awe na weledi wa kutosha juu ya mbinu za kusimulia hadithi. Mbinu hozo ni hizi;
A) Dhima na maudhui
Msimuliaji wa hadithi anapaswa kujua lengo kuu (dhima) la hadithi yake. Vilevile msimuliaji anapaswa kujua maudhui ambayo ni jumla ya mambo yote yanayopelekea hadithi kutiririka vizuri kwenye mkondo wake.
B) Msuko
Msuko wa matukio kwa jina jingine unafahamika kama muundo. Kipengele hiki cha muundo kinahusu mpangilio wa hadithi kuanzia mwanzo mpaka mwisho.
C) Kusisimua
Kusisimua ni mbinu inayovuta umakini kwa watu. Msimuliaji anaweza kutumia mbinu kadhaa zitakazo msisimusha msomaji, mbinu kama vile taharuki, miguno na kelele za kutisha.
D) Urudufishaji
Huu ni urudiaji rudiaji katika fasihi simulizi. Mara nyingi msimuliaji anashauriwa kurudia rudia maneno, falsafa, nahau au vitendawili vilivyobeba lengo kuu la hadithi yake.
E) Chombezo
Chombezo ni kipengele kidogo kinacho elezwa na mtambaji wa hadithi chenye lengo la kupunguza ukakasi ama ukalia ama vitisho vilivyotokana na maudhui ya hadithi Fulani.
F) Nyimbo
Nyimbo zina kazi nyingi katika masimulizi ya hadithi. Moja wapo ya matumizi hayo ni kama vile kuondoa uchovu kwa wasikilizaji, kuvuta usikivu, kuwakaririsha hadhira falsafa au lengo kuu la hadithi hiyo.
MAMBO MENGINE
a) Utulivu kwa hadhira
b) Ujenzi wa wahusika
c) Matumizi ya tamathali za semi
d) Ujenzi wa taswira
2. FASIHI ANDISHI
Williady (2015) fasihi andishi ni aina ya fasihi inayowasilishwa kwa ustadi wa maandishi yenye kuleta maana.
Wamitila (2004) fasihi andishi ni sanaa inayowasilishwa kwetu kwa maandishi.
TANZU ZA FASIHI ANDISHI
RIWAYA (NATHARI)
USHAIRI (NUDHUMU)
TAMTHILIYA (SANAA ZA MAONYESHO)
FANI NA MAUDHUI KATIKA FASIHI
Fani na maudhui katika fasihi ndio maumbo mawili makuu yanayobeba sanaa hii.
FANI
Fani ni ufundi unaotumiwa na msanii katika kufikisha ujumbe uliokusudiwa, fani sio ujumbe bali ni mfano wa kipaza sauti kinachotumika kufikisha ujumbe.
VIPENGELE VYA FANI
Fani inavipengele vingi, kila kipengele kina husika kipekee kwa kutofautiana na kipengele kingine.
Vipengele vya fani ni pamoja na;
a) Muundo
Kipengele hiki hutumiwa kueleza mpangilio wa kazi ya kifasihi. Kwa ufupi kwenye kipengele cha muundo tunaangalia umbo la kazi ya fasihi, mfano kazi yaweza kugawanywa katika sura mbalimbali, sura hizi ndizo ujenga muundo.
b) Mtindo
Williady (2015) mtindo ni mbinu za kipekee zinazomtofautisha msanii mmoja na mwingine. Mfano katika fasihi simulizi kipengele cha nyimbo hadhira inaweza kusikia wimbo kwa mara ya kwanza na kutambua wimbo huo umeimbwa na nani bila ya kuambiwa na mtangazaji, hii huweza kutokea pindi mwimbaji mashuhuri anayetumia mtindo wa peke yake katika sauti na mpangilio wa mashairi anapotoa wimbo mpya. Huu ndio huitwa mtindo. Katika fasihi andishi mtindo unaweza kujitokeza kwa njia za kipekee za mtunzi katika matumizi ya lugha, methali na misemo, msuko na mpangilio wa vina na mizani katika ushairi.
c) Mandhari
Williady (2015) Mandhari ni eneo au mazingira ya kweli au yakubuni ambayo hutumiwa na mwandishi katika kuwajenga wahusika na uhusika wao.
d) Matumizi ya Lugha
Williady (2015) Matumizi ya lugha ni ustadi wa msanii katika kutumia lugha itakayoleta mvuto kwa wasomaji au wasikilizaji wa kazi ya fasihi.
Katika kutumia lugha msanii lazima azingatie kipengele cha uteuzi wa maneno yanayoendana na hadhira yake, maneno hayo ndiyo yatakayoleta mfungamanisho katika ya msanii, hadhira na ujumbe uliokusudiwa.
e) Matumizi ya tamathali za semi(usemi)
Williady (2015) Tamathali maanayake ni neon moja au kifungu cha maneno kilicho sukwasukwa na kufichwa maana.
Baadhi ya tamathali za semi katika Kiswahili ni pamoja na;
Tashibiha, sitiari, tafsida, tashihisi, chuku, kinaya,dhihaka, mbalagha,tabaini
f) Mbinu nyingine za kisanaa
Hapa huwa na mchanganyiko wa mbinu kadhaa katika usimulizi na silazima mbinu hizo zitumike zote kwa wakati mmoja. Mfano wa mbinu hizo ni pamoja na;
Takriri, kuchanganya ndimi, tanakali sauti, taswira, lakabu, nahau na misemo
Takriri, kuchanganya ndimi, tanakali sauti, taswira, lakabu, nahau na misemo
e) Wahusika
Williady (2015) wahusika ni viumbe hai au viumbe ambao si hai wanaobebeshwa majukumu na msanii ili kuwafikishia hadhira ujumbe uliokusudiwa.
MAUDHUI KATIKA FASIHI SIMULIZI
(williady: 2015) Maudhui ni jumla ya mawazo anayoyazungumzia msanii au mtunzi katika kazi ya fasihi.
Maudhui hujumuisha vipengele mbalimbali, kama vile;Dhamira, ujumbe, falsafa, mafunzo, migogoro na mtazamo.
TANBIHI: Kuna baadhi ya wataalamu wa lugha wanakiweka kipengele cha migogoro upande wa fani na kunabaadhi wanakiweka kipengele hiki upande wa maudhui. Mimi nakiweka upande wa maudhui kwa kuwa migogoro inabeba kwa kiasi kikubwa ujumbe kuliko ufundi.
DHAMIRA
Dhamira ni shabaha kuu ya mtunzi wa kazi ya fasihi. Shabaha hii ukusudiwa ni nani wakumlenga nayo. Msanii anaweza kuwalenga kimaudhui watoto, wanawake, wasomi au watu wote katika jamii. Shabaha hii yaweza kuandikwa au kutongolewa kwa mdomo ikiwa na lengo la kupongeza, kuhimiza, kushauri, kutoa taarifa na kukosoa.
UJUMBE
Ujumbe ni mawazo yanayotokana na dhamira, mawazo haya yaweza kujitokeza waziwazi au kwa kificho.
FALSAFA
Falsafa ni hekima hekima ya mtunzi. Mtunzi huamini kuwa kupitia imani hii jamii inaweza kupata suluhisho la matatizo yanayowakabili. Kwa mfano shekhe Shaaban Robert aliamini kuwa kila mwanajamii akiwa na utu basi haki na upendo vitapatikana kirahisi.
MAFUNZO
Mafunzo ni nasaha anazotoa mtunzi ambazo huifundisha hadhira maadili Fulani. Maana ya mafunzo hutegemea namna hadhira inavyofasili nasaha hizo.
MIGOGORO
Migogoro ni misuguano au mikinzano ama kutoelewana kati ya pande mbili au zaidi ndani ya kazi za fasihi.
AINA ZA MIGOGORO
Mgogoro kati ya mtu na mtu
Mgogoro kati ya mtu na jamii
Mgogoro kati ya jamii na jamii
Mgogoro wa nafsi
VI. MTAZAMO
Mtazamo na jinsi mwandisi anavyotazama na kuyachukulia matukio katika ulimwengu na athari zake kwa wanajamii. Mfano waandishi wengi wa mashairi wanamtazamoa huu “Kuibuka kwa maovu mengi duniani kwasasa ni matokeo ya binadamu.
METHALI ZA KISWAHILI
ZIMEKUSANYWA NA MWL. MAJUMBENI
Methali ni nyenzo ya msingi katika makuzi ya fasihi ya Kiswahili. Tangu kale Methali zimetumika katika kujenda jamii kwa kutoa maonyo na kuambukika tabia njema hasa kwa vijana wanaochipukia.
Wataalamu wengi wameeleza maana ya Methali, lakini maana halisi bado inaendelea kushabihiana japokuwa kuna mikinzano katika baadhi ya maeneo. Maana halisi ya methali itabaki kuwa,
“Methali ni kipera cha semi katika fasihi simulizi kinachojengwa kwa pande mbili, pande moja ni yenye kuuliza swali na nyingine yenye kujibu swali zikiwa na lengo la kufunza amali za jamii kwa vijana.
Zifuatavyo ni baadhi ya METHALI , zikiwa vimepangwa ki - alfabeti:
“A”
1. Adhabu ya kaburi aijua maiti
2. Adui mpende
3. Aibu ya maiti aijua mwosha
4. Aisifuye mvua imemnyea
5. Ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke
6. Achambaye na gunzi hatakatiki
7. Akimbiaye mvua, akimbia shibe
8. Akiba haiozi
9. Akili ni mali
10. Akili ni nywele kila mtu ana zake
11. Akili nyingi huondoa maharifa
12. Akipenda chongo, huita kengeza
13. Akumulikaye mchana, usiku akuchoma
14. Akutendaye mtende mche asiyekutenda
15. Anaekula kibudu, ashibisha tumbo wala si nafsi
16. Alalaye usimwamshe, ukimwamsha utalala wewe
17. Alisifiye jua, limemwangaza
18. Aliye kando haangukiwa na mti.
19. Aliyekupa wewe kiti, ndiye aliyenipa mimi kumbi
20. Aliyetota, hajui kutota
21. Amani haipatikani ila kwa ncha ya upanga
22. Amnyimaye punda adesi, kampunguzia mashuzi
23. Ana hasira za mkizi
24. Anayekataa wengi ni mchawi
25. Amtukanaye jumbe hafikwi na kesi
26. Anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi na kuaga
27. Anayeonja asali, huchonga mzinga
28. Anayetaka hachoki hata akichoka keshapata
29. Angakaanga, tu chini agae
30. Angenda juu kipanga, hafiki mbinguni
31. Angurumapo simba, mcheza nani?
32. Aninyimaye mbaazi, kanifunguzia mashuzi
33. Atupaye kopo la choo, hafikwi na haja
34. Apewaye ndie aongezwaye
35. Asiye bahati habahatiki / habahatishi
36. Asiyefunzwa na mamaye, hufunzwa na ulimwengu
37. Asiyejua jua maana, haambiwi maana
38. Asiyekujua hakudhamini
39. Asiyekubalikushindwa si mshindani
40. Asiyekuwapo machoni, na moyoni hayupo
41. Asiyekuwapo na lake halipo
42. Asiye na mengi, ana machache
43. Asiye na meno, hapewi nyama ya kiuno
44. Asiyesikia la mkuu, huvunjika guu
45. Asiyeuliza, hanalo ajifunzalo
46. Atangaye sana na jua, hujua
47. Atangazaye mirimo si mwana wa ruwari
48. Auguwaye, huangaliwa
49. Avuaye nguo, huchutama
50. Avumaye bahariki papa (kumbe wengine wapo)
“B”
51. Baada ya dhiki, faraja
52. Baada ya kisa, mkasa
53. Baada ya chanzo, kitendo
54. Baba wa kambo si baba
55. Bandu! Bandu! Huisha gogo
56. Baniani mbaya, kiatu chake dawa
57. Bendera hufuata upepo
58. Bembea umpa raha apendae
59. Bilisi wa mtu ni mtu
60. Bura yangu sibadili na rehani
“C”
61. Cha mlevi huliwa na mgema
62. Chanda chema huvikwa pete
63. Chema chajiuza, kibaya chajitembeza
64. Chombo cha kuzama hakina usukani
65. Chombo kilichopikiwa samaki, hakiachi kunuka vumba
66. Chovya – chovya! Yamaliza buyu la asali
67. Chururu si ndo!ndo !ndo
68. Dalili ya mvua ni mawingu
69. Damu nzito kuliko maji
70. Dau la mnyonge halendi joshi
71. Dawa ya moto ni moto
72. Debe tupu haliachi kuvunda
73. Dua la kuku halimpati mwewe
74. Dua mbaya haombolezewi mtoto
“E”
75. Elimu ni bahari
76. Ellimu ni ufunguo, haina mwisho
77. Elimu ya mjinga ni majungu
“F”
78. Fadhili za punda, mashuzi, na msihadhari ni ng’ombe
79. Fimbo iliyo mkononi, ndiyo iuayo nyoka
80. Fimbo ya mbali, haiui nyoka
81. Fuata nyuki, ule asali
82.Fumbo mfumbie mjinga, mwerevu hulingamua
83. Fungato haliumizi kuni
84. Funika kombe mwanaharamu apite
“G”
85. Ganda la mua la jana, chungu kaona kivuno
86. Gonga gogo usikilize mlio wake
87. Gonga! Gonga! utoka cheche
“H”
88. Haba na haba hujaza kibaba
89. Halla! Halla! Mti na macho
90. Hamadi, kibindoni, silaha, iliyo mkononi
91. Hamna! Hamna! Ndimo mlimo
92. Hapana marefu yasiyo na ncha
93. Hapana masika yasiyo na mbu
94. Hapana msiba usiokuwa na mwenziwe
95. Hapana siri ya watu wawili
96. Hapana ziada mbovu
97. Haraka haraka haina Baraka
98. Hasara humfika mwenye mabezo
99. Hasira, hasara
100. Hauchi – hauchi unakucha
101. Hayawi! Hayawi! Huwa
102. Heri kufa macho kuliko kufa moyo
103. Heri kufa mwili kuliko kufa roho
104. Heri kujikwaa dole, kuliko kujikwaa ulimi
105. Heri nusu ya shari kuliko shari kamili
106. Hewalla! Haigombi
107. Hiari yashinda utumwa
108. Hucheka kovu, asiyefikiwa na jeraha
109. Hakunyimae tonge, hakunyimi neon
“I”
110. Ihsani haiozi
111. Ikiwa hujui kufa, tazama kaburi
112. Iliyopita si ndwele, ganga ijayo
113. Ivushayo ni mbovu
114. Ivumayo haidumu ikidumu inamkono wa mtu
115. Iwapo nia, njia hupatikana
“J”
116. Jicho moja halizuii kutazama uchi
117. Jifya moja haliinjiki chungu
118. Jina jema hung’aa gizani
119. Jino la pembe si dawa yap ego
120. Jitihada haiondoi kudura
121. Jongoo hulia “uta wangu u kule”
122. Jogoo la shamba haliwiki mjini
123. Joka la mdimu linalinda watundao
124. Jungu bovu limekuwa magae
125. Jungu kuu halikosi ukoko
“K”
126. Kafiri akufaaye si Islamu asiyekufaa
127. Kamba hukatikia pembamba
128. Kanga moja, haistiri maungo
129. Kanga iliyotota, Uganda maungo
130. Kanga hazai ugenini
131. Kata pua, unga wajihi
132. Kawaida ni kama sheria
133. Kawia ufike
134. Kazi mbaya si mchezo mwema
135. Kelele za mlango haziniwasi usingizi
136. Kenda karibu na kumi
137. Kiburi si maungwana
138. Kichango, huchangizana
139. Kidole kimoja hakivunji chawa
140. Kiingiacho mjini si haramu
141. Kikulacho ki nguoni mwako
142. Kila chombo kwa wimbile
143. Kila mlango kwa ufunguo wake
144. Kila mtoto na koja lake
145. Kila mwamba ngoma, ngozi huivuta kwake
146. Kila ndege huruka kwa bawa lake
147. Kilio huanza mfiwa, ndipo na wa mbali wakaingia
148. Kimya kingi kina mshindo
149. Kinga na kinga ndipo moto uwaka
150. Kinyozi hajinyoi na akijinyoa hujikata
151. Kinywa ni jumba la maneno
152. Kipendacho roho hula nyama mbichi
153. Kipendacho moyo ni dawa
154. Kipya kinyemi, ingawa kidonda
155. Kisebusebu na kiroho papo
156. Kisokula mlimwengu, sera nale
157. Kitanda usichokilala, hujui kunguni wake
158. Kivuli cha fimbo hakimfichi mtu jua
159. Kivuli cha mvumo huwafunika walio mbali
160. Kiwi cha Yule, ni chema cha Yule, hata ulimwengu wishe
161. Kizuri chajiuza, kibaya chajitembeza
162. Koko haidari mai
163. Konzi ya maji haifumbatiki
164. Kosa moja haliachi mke
165. Kozi mwana mandanda, kulala na njaa kupenda
166. Kuagiza, kufyekeza
167. Kuambiana kupo, kusikilizana hapana
168. Kucha Mungu si kilemba cheupe
169. Kuchamba kwingi kuondoka na mavi
170. Kufa kikondoo, ndiko kufa kiungwana
171. Kufa, kufaana
172. Kufa kwa jamaa, harusi
173. Kufa kwa mdomo, mate hutawanyika
174. Kuishi kwingi ni kuona mengi
175. Kujikwaa si kuanguka, bali ni kwenda mbele
176. Kukopa harusi, kulipa matanga
177. Kuku havunji yayile
178. Kuku mwenye watoto halengwi jiwe
179. Kula kutamu, kulima mavune
180. Kulea mimba si kazi kazi kulea mwana
181. Kulenga si kufuma
182. Kumla ngulu si kazi, kazi kumwosha
183. Kunako matanga, kumekufa mtu
184. Kunguru mwoga hukimbiza bawa lake
185. Kupanda mchongoma kushuka ngoma
186. Kupotea njia ndiko kujua njia
187. Kutoa ni moyo usambe ni utajiri
188. Kutu kuu ni la mgeni
189. Kutwanga nisile unga, nazuia mchi wangu
190. Kuzima koleo si mwisho wa uhunzi
191. Kwa mwoga huenda kicheko kwa shujaa huenda kilio
192. Kwenda mbio si kufika
193. Kwenye miti hakuna wajenzi
“L”
194. La kuvuma halina ubani
195. La kuvunda halina ubani
196. Lake mtu halumtapishi bali humchefua
197. Leo ni leo asemaye kesho ni mwongo
198. Liandikwalo ndilo liwalo
199. Lila na fila hazitangamani
200. Lipitalo, hupishwa
201. Lisemwalo lipo, ikiwa halipo, lipo nyuma linakuja
202. Lisilokuwepo moyoni halipo machoni
“M”
203. Maafuu hapatilizwi
204. Macho hayana pazia
205. Mafahali wawili hawakai zizi moja
206. Maiti haulizwi sanda
207. Maiti hachagui sanda
208. Maji hufuata mkondo
209. Maji huteremkia bondeni, hayapandi kilimani
210. Maji ukiyavulia nguo huna budi kuyaoga
211. Maji usiyofika hujui wingi wake
212. Maji ya kifuu ni bahari ya chungu
213. Maji yakimwagika hayazoleki
214. Majumba makubwa husitiri mambo
215. Majuto ni mjukuu, mwishowe huja kinyume
216. Mambo kikowa
217. Manahodha wengi chombo huenda mpera
218. Maneno mema humtoa nyoka pangoni
219. Maneno makali hayavunji mfupa
220. Mapenzi ni kikohozi, hayawezi kufichika
221. Maskini akipata, matako hulia mbwata
222. Maskini na mwanawe, tajiri na mali yake
223. Mavi usiyala, wayawingiani kuku?
224. Mavi ya kale hayanuki
225. Mbaazi ukikosa maua, husingizia jua
226. Mbinu hufuata mwendo
227. Mbio za sakafuni, huishia ukingoni
228. Mbiu ya mgambo ikilia ina jambo
229. Mchagua jembe si mkulima
230. Mchagua nazi, hupata koroma
231. Mchakacho hujao, haulengwa na jiwe
232. Mchama ago hanye hanyeli, huenda akauya papo
233. Mchelea mwana kulia, hulia yeye
234. Mchele mmoja, mapishi mengi
235. Mcheka kilema hafi bila kumfika
236. Mcheza hawi kiwete, ngoma yataka matao
237. Mcheza kwao hutunzwa
238. Mcheza na tope humrukia
239. Mchimba kisima, hakatazwi maji
240. Mchimba kisima huingia mwenyewe
241. Mchimba kisima humtia mtuwe
242. Mchonga mwiko hukimbiza mikono yake
243. Mchovya asali hachovyi mara moja
244. Mchuma janga hula na wakwao
245. Mchumia juani hula kivulini
246. Mdharau mwiba mguu huota tende
247. Mdharau biu, hubiuka yeye
248. Meno ya mbwa hayaumani
249. Mfa maji hukamata maji
250. Mficha uchi hazai
251. Mfinyanzi hulia gaeni
252. Mfuata nyuki hakosi asali
253. Mfukuzwa kwao hana pa kwenda
254. Mgaagaa na upwa hali wali mkavu
255. Mganga hajigangi
256. Mgema akisifiwa Tembo hulitia maji
257. Mgeni hachomi chaza mtaani akanuka
258. Mgeni ni kuku mweupe
259. Mgeni njoo mwenyeji apone
260. Mgonjwa haulizwi uji
261. Miye nyumba ya udogo, sihimili vishindo
262. Mja hana hiari
263. Mkamatwa na ngozi ndiye mwizi
264. Mkamia majihayanywi, akiyanywa humpalia
265. Mkata hana kinyongo
266. Mkata hapendi mwana
267. Mkate mkavu wa nyumbani ni bora kuliko nyama ya shuwa yap engine
268. Mke ni nguo, mgomba kupalilia
269. Mkono mmoja hauchinji ng’ombe
270. Mkono mmoja haulei mwana
271. Mkono mtupu haulambwi
272. Mkono usioweza kuukata, ubusu
273. Mkosa kitoweo, humangilia
274. Kabuki kwa nguruwe, kwa binadamu mchungu
275. Mkulima ni mmoja, walaji ni wengi
276. Mla cha mwenziwe na chake huliwa
277. Mla cha uchungu na tamu hakosi
278. Mla kuku wa mwenziwe miguu humwelekea
279. Mla mbuzi hulipa ng’ombe
280. Mla kwa miwili hana mwisho mwema
281. Mla, mla leo, mla jana kala nini?
282. Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe
283. Mlenga jiwe kundini hajui limpataye
284. Mlilala handingwadingwa, mwenye macho haambiwi tule
285. Mlimbua nchi ni mwananchi
286. Mnyamaa kadumbu
287. Mnywa maji kwa mkono mmoja, kiu yake I pale pale
288. Moja shika si kumi nenda uje
289. Moto hauzai moto
290. Mpanda farasi wawili, hupasuka msamba
291. Mpanda ovyo, hula ovyo
292. Mpemba akipata gogo, hanyi chini
293. Mpemba hakimbii mvua ndogo
294. Mpemba hashoni tomo dogo
295. Mpiga ngumi ukutani huumiza mkonoe
296. Mpofuka uzeeni hapotei njia
297. Msafuri kafiri
298. Msafiri maskani, ajapokuwa sultani
299. Msasi haogopi miiba
300. Msema pweke, hakosi
301. Mshare kwenda msituni haukupotea
302. Mshoni hachagui nguo
303. Msitukane wagema na ulevi ungalimo
304. Msitukane wakunga na uzazi ungalimo
305. Mstahimivu, hula mbivu
306. Mtaka cha uvunguni huinama
307. Mtaka nyingi nasaba hupata nwingi msiba
308. Mtaka nyingi faida husogeza nyingi hasara
309. Mtaka yote hukosa yote
310. Mtaka hunda haneni
311. Mtegemea nundu haachi kunona
312. Mtegemea ndugu hufa masikini
313. Mtembezi hula miguu yake
314. Mteuzi haishi tama
315. Mti hawendi ila kwa nyenzo
316. Mtondoo haufi maji
317. Mtoto akibebwa hutazama kisogo cha mamaye
Kama wewe ni mtafiti au mdau wa Kiswahili unataka kujua kuhusu methali au unahitaji methali vingi zaidi kwa matumizi ya kufundishia au kuandika tasnifu, tafadhali wasiliana nami kwa,
0759392855
0676392856
Onesha marejeleo mwixho wa kazi yko
ReplyDeleteMarejeleo huna? Si rahisi mtu kuchukua mawazo yako
ReplyDelete