Skip to main content

RIWAYA YA MOTO WA MIANZI

MOTO WA MIANZI
MAUDHUI
SWALI:  Chambua Maudhui ya Riwaya ya Moto wa Mianzi
Historia fupi ya Mwandishi na utunzi wa kazi yake:
RIWAYA YA MOTO WA MIANZI; ni riwaya iliyoandikwa na mwandishi aitwaye Mugyabuso Mulokozi. Alizaliwa tarehe 7 Juni mwaka 1950. Mugyabuso Mulokozi ni muhadhiri katika chuo kikuu cha Dar es Salaam. Mwandishi huyu pia ameweza kuandika kazi mbalimbali. Baadhi ya kazi zake ni:
·         Mashairi ya kisasa aliyoandika kwa kushirikiana na K.K Kahigi.
·         Malenga wa Bara aliyoandika pamoja na K.K Kahigi
·         Mukwava wa Uhehe
·         Kunga za Ushairi na Diwani yetu aliyoandika pamoja na K.K Kahigi
·         Ngome ya Mianzi
·         Ngoma  ya Mianzi
Tukirejea zaidi riwaya ya Moto wa Mianzi; riwaya hii inahusu matukio yaliyofuatia kutekwa kwa ngome ya Kalenga mwaka 1894. Katika riwaya hii Mutwa Mukwawa alikimbila Kilolo kwa baba yake. Mugoha Muhanzala, Nyawelu wakiwa na mtoto Semuganga walipewa jukumu la kumpeleka Sapi bin Mukwava, Kilolo kwa baba yake. Mwandishi anajadili masaibu yaliyowapata njiani.
Riwaya ya Moto wa Mianzi  ni ainaya riwaya ya kimajaribio kwa kuzingatia kigezo cha fani kutokana na kwamba imetumia kanuni ambazo si zoefu katika utanzu wa riwaya kwa mfano kwenye kipengele cha fani na maudhui. Riwaya nyingine zinazofanana na riwaya husika kimaudhui ni kama vile Nagona na Mzingile.                                                                                                       Kutokana na swali ambalo limejikita zaidi katika maudhui, dhana ya maudhui ni pana. Maudhui  ni mawazo au mambo yanayosemwa ndani ya kazi ya sanaa.Maudhui yanaweza kuwa jambo lolote  linalomkera mwanadamu , kwa mfano maana ya maisha, mapenzi, mauti, ndoa, elimu, kazi, ukombozi, dini, nk.Maudhui hujumuisha mawazo pamoja na mafunzo mbalimbali yaliyomsukuma msanii hadi akatunga na kusanii kazi fulani ya kifasihi.Vipengele vya maudhui ni pamoja na dhamira, migogoro, falsafa, ujumbe na msimamo wa mwandishi.
Dhamira
Dhamira ni malengo/lengo/wazo kuu la mwandishi katika kazi ya fasihi. Zifuatazo ni dhamira chomozi katika riwaya ya Moto wa Mianzi.
Dhamira kuu
Ukombozi wa kifikra, Wanyigendo waliweza kujitambua kuwa wananyanyaswa na Wadachi na kuanza kutafuta njia ya kijikomboa kutoka mikononi mwa Wadachi. Waliweza kuwa na umoja wa dhati kwa mfano walishirikiana kijiji kimoja hadi kingine kuwapokea waliojitoa mhanga ili kumwokoa Sapi ambaye alikuwa na  Mugoha pamoja na Nyawelu. Sapi alikuwa anatafutwa na Wadachi ili wamnyonge lakini Mugoha,  Nyawelu na Wanyigendo waliweza kushirikiana ili kumwokoa Sapi. Mfano Wanyigendo waliwapokea Mugoha, Nyawelu na Sapi (uk. 14) kutoka kijiji cha Ipamba na kupokelewa Idegesi (uk.22). Hii ilionyesha walikuwa na ushirikiano baada ya kujitambua ili kumwokoa Sapi na waliweza kutumia alama mbalimbali kutoa taarifa kwa wale waliokuwa wanasafiri kwenda Kilolo, na walitumia alama za kufunga nyasi mafundo mafundo na kuyapanga njiani ili kutoa taarifa kuwa hali sio nzuri.Ukombozi wa kisiasa,
Ukombozi wa kisiasa, Ni kujikomboa kiitikadi ambapo itikadi moja inapingana na itikadi nyingine na kusababisha hali ya mvutano kati ya  matabaka. Katika riwaya hii mwandishi amefanikiwa kuonyesha ukombozi wa kisiasa uliokuwa  unafanywa na Wahehe ili kupata uhuru katika jamii zao.
Ujasiri na kujitoa mhanga
Ni hali ya mtu au watu wachache kukubali kujitoa kwa ajili ya wengi,a kwa ajili  liwaya hii wamejitokeza wahusika walio weza kujitoa muhanga kwa ajili ya watu wao mwandishi ameweza kumtumia muhusik Mugoha aliyejitolea kukamatwa na wadachi na kujiita Sapi ili aweze kumuokoa Sapi. Hii tunapata katika ukurasa wa 72 Mugoha anasema                                       “Nataka kuwahadaa. Hakuna njia nyingine”                                                                                                                “Utawahadaaje?Alizidi kuuliza.                                                                                       “Nitawaendea na kuwaambia kuwa mimi ndiye Sapi”
Pia katika ukuras wa 86-87  ujasili wa Mugoha unaendelea kujidhihilisha alipo ambiwa na Sapi baada ya kukutana nae gerezani anasema. Ni hivi, wewe ulipoamua kujitoa kwa Wadachi kwa niaba yetu, ulifanya uamuzi wa kujitoa muhanga kutoa maisha yako kwa niaba yetu. Bahati mbaya  nilikuwa usingizini  hivyo ni kama sikuwepo. Ningekuwepo nisingekubali uchukue hatua hiyo” Katika jami zetu za sasa za kitanzania na Africa kwa ujumla, wapo watu ambao hujitolea maisha yao kwa ajili ya kukomboa maisha ya ya watu walio wengi licha ya kwamba huweza kukumbana na vizingiti vingi na wengine huishia kufa au kufungwa magerezan lakini lengo ikiwa ni kuwakomboa wanajamii
Usaliti

Comments

Popular posts from this blog

KISWAHILI FORM 1: FASIHI SIMULIZI

KISWAHILI Form 1 Topic 4 FASIHI SIMULIZI Fasihi simulizi ni moja kati ya tanzu za fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo. Katika mada hii utajifunza na kisha utaweza kubainisha tanzu na vipera vya fasihi simulizi pamoja na ufafanuzi wake. Na pia utaweza kutofautisha kati ya kipera na kipera au kati ya utanzu na utanzu. Ubainishaji wa Tanzu za Fasihi Simulizi Tanzu za Fasihi Simulizi Bainisha tanzu za fasihi simulizi Fasihi Simulizi ni kazi ya fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo kama vile; hadithi, ngoma na vitendawili. Tanzu za Fasihi Simulizi ni pamoja na hizi zifuatazo: Masimulizi/hadithi Semi Ushairi Mazungumzo Maigizo Ngomezi Ufafanuzi wa Vipera vya Tanzu za Fasihi Simulizi Vipera vya Hadithi Fafanua vipera vya hadithi SIMULIZI/ HADITHI Masimulizi ni fasihi yenye kusimulia habari fulan...

NOTES ZA USHAIRI

USHAIRI     NI    NINI ? Shaaban Robert katika uandishi wa ushairi ameandika Tenzi na mashairi ya kimapokeo. Tenzi : Ni aina ya mashairi ya kimapokeo wenye sifa zifuatazo: Kimaudhui ; Ni utungo wenye maudhui yanayosimulia kwa urefu tukio fulani maalum. Waweza kuwa wasifu wa mtu au jambo la kihistoria. Mfano; S. Robert ameandika utenzi wa vita vya Uhuru, ameeleza kuhusu historia. Pia katika Mapenzi Bora, ameeleza kuhusu sifa za mapenzi bora. Utenzi ni utungo wa pili kati tungo za ushairi zenye beti nyingi. Utungo wa kwanza unaoongoza kuwa na beti nyingi kuliko zote katika ushairi ni Tendi. Lakini hapa tutaangazia tenzi zaidi. Utenzi hauna mizani nyingi aghalabu mizani nane, hauna mshororo bali una nusu mshororo/kipande mstari. Vilevile katika utenzi kipande mstari hakigawiki. Pia katika kipande mshororo kuna vipande vinne kwa kila ubeti. Mistari mitatu ya kwanza huwa na vina vyenye urari na kipande mstari cha mwisho/cha nne huwa...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

Mbinu za kufundishia , ni miongozo mbalimbali atumiayo mwalimu wakati wa kufundisha somo aliloliandaa kwa wanafunzi wake. Walimu wanapaswa kuamua kwa kuchagua kwa makini njia na mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Ziko njia nyingi za kutengeneza mazingira ya mtoto aweze kujifunza na pia ziko mbinu nyingi za kufundishia. Pamoja na wingi huo tunaweza kuzigawa katika makundi makuu mawili kadri ya jinsi zinavyowashirikisha watoto katika tendo la kujifunza, ambazo tunaweza kuziita shirikishi na zisizo shirikishi . Zifuatazo ni baadhi ya mbinu shirikishi na zisizo shirikishi za kufundishia pamoja na faida na hasara zake:- Njia ya majadiliano , njia hii imekuwa ikitumika katika ufundishaji kwa muda mrefu. Katika kujadiliana mwanafunzi mmoja mmoja hupata nafasi ya mawazo aliyonayo kuhusu suala linalojadiliwa na yeye pia huweza kupata mawazo yaw engine. Katika majadiliano mwanafunzi hupata ujuzi mpya nje na ule aliokuwa nao kabla hajashiriki kat...