Skip to main content

SHAIRI: NI KIPELE AMA JIPU CHANGA


Kama ndiko kufanana,ni zaidi ya mayai,
Unaweza kugombana,jibu lako kulidai,
Si urefu si upana,kasoro huing'amui,
NI KIPELE JIPU CHANGA,WALIMU NIAMBIENI.

Wapo walopata sifa,kudai ni jipu changa,
Nasi wasaka marifa,twashindwa kipi kulonga,
Vichwa vinapata nyufa,fikra zikijigonga,
NI KIPELE JIPU CHANGA,WALIMU NIAMBIENI.

Wengine ni kaupele,kovu lake halidumu,
Wala huhitaji shule,wala siyo jambo gumu,
Hutotoa ukelele,kukamua siyo sumu,
NI KIPELE JIPU CHANGA,WALIMU NIAMBIENI.

Huenda likawa jipu,tusubiri tukajua,
Sije sema chupu chupu,jipu lingejiotea,
Na msindi tumpe supu,jibu akilipatia, 
NI KIPELE JIPU CHANGA,WALIMU NIPENI JIBU.

Jipu huliacha kovu,kovu kubwa la kidonda,
Kama macho ni mabovu,tapapasa ukipenda,
Ama kwa wako uchovu,uliza acha kuponda,
NI KIPELE JIPU CHANGA,WALIMU NIAMBIENI.

Wengine ni kaupele,kovu lake halidumu,
Wala huhitaji shule,wala siyo jambo gumu,
Hutotoa ukelele,kukamua siyo sumu,
NI KIPELE JIPU CHANGA,WALIMU NIAMBIENI.

Huenda likawa jipu,tusubiri tukajua,
Sije sema chupu chupu,jipu lingejiotea,
Na mshindi tumpe supu,jibu akilipatia, 

NI KIPELE JIPU CHANGA,WALIMU NIPENI JIBU

Comments

Popular posts from this blog

KISWAHILI FORM 1: FASIHI SIMULIZI

KISWAHILI Form 1 Topic 4 FASIHI SIMULIZI Fasihi simulizi ni moja kati ya tanzu za fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo. Katika mada hii utajifunza na kisha utaweza kubainisha tanzu na vipera vya fasihi simulizi pamoja na ufafanuzi wake. Na pia utaweza kutofautisha kati ya kipera na kipera au kati ya utanzu na utanzu. Ubainishaji wa Tanzu za Fasihi Simulizi Tanzu za Fasihi Simulizi Bainisha tanzu za fasihi simulizi Fasihi Simulizi ni kazi ya fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo kama vile; hadithi, ngoma na vitendawili. Tanzu za Fasihi Simulizi ni pamoja na hizi zifuatazo: Masimulizi/hadithi Semi Ushairi Mazungumzo Maigizo Ngomezi Ufafanuzi wa Vipera vya Tanzu za Fasihi Simulizi Vipera vya Hadithi Fafanua vipera vya hadithi SIMULIZI/ HADITHI Masimulizi ni fasihi yenye kusimulia habari fulan...

NOTES ZA USHAIRI

USHAIRI     NI    NINI ? Shaaban Robert katika uandishi wa ushairi ameandika Tenzi na mashairi ya kimapokeo. Tenzi : Ni aina ya mashairi ya kimapokeo wenye sifa zifuatazo: Kimaudhui ; Ni utungo wenye maudhui yanayosimulia kwa urefu tukio fulani maalum. Waweza kuwa wasifu wa mtu au jambo la kihistoria. Mfano; S. Robert ameandika utenzi wa vita vya Uhuru, ameeleza kuhusu historia. Pia katika Mapenzi Bora, ameeleza kuhusu sifa za mapenzi bora. Utenzi ni utungo wa pili kati tungo za ushairi zenye beti nyingi. Utungo wa kwanza unaoongoza kuwa na beti nyingi kuliko zote katika ushairi ni Tendi. Lakini hapa tutaangazia tenzi zaidi. Utenzi hauna mizani nyingi aghalabu mizani nane, hauna mshororo bali una nusu mshororo/kipande mstari. Vilevile katika utenzi kipande mstari hakigawiki. Pia katika kipande mshororo kuna vipande vinne kwa kila ubeti. Mistari mitatu ya kwanza huwa na vina vyenye urari na kipande mstari cha mwisho/cha nne huwa...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

Mbinu za kufundishia , ni miongozo mbalimbali atumiayo mwalimu wakati wa kufundisha somo aliloliandaa kwa wanafunzi wake. Walimu wanapaswa kuamua kwa kuchagua kwa makini njia na mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Ziko njia nyingi za kutengeneza mazingira ya mtoto aweze kujifunza na pia ziko mbinu nyingi za kufundishia. Pamoja na wingi huo tunaweza kuzigawa katika makundi makuu mawili kadri ya jinsi zinavyowashirikisha watoto katika tendo la kujifunza, ambazo tunaweza kuziita shirikishi na zisizo shirikishi . Zifuatazo ni baadhi ya mbinu shirikishi na zisizo shirikishi za kufundishia pamoja na faida na hasara zake:- Njia ya majadiliano , njia hii imekuwa ikitumika katika ufundishaji kwa muda mrefu. Katika kujadiliana mwanafunzi mmoja mmoja hupata nafasi ya mawazo aliyonayo kuhusu suala linalojadiliwa na yeye pia huweza kupata mawazo yaw engine. Katika majadiliano mwanafunzi hupata ujuzi mpya nje na ule aliokuwa nao kabla hajashiriki kat...