Skip to main content

SHAIRI: NI TAA YA AFRICA

Yang'aa kila dakika, na kuburudisha moyo,
Wachache waaliofika, umewatoka uchoyo,
Yeyote atamwalika, akaliwazike moyo,

Hii taa ya labuka, kaiweka hapa kwetu,
Ni kama kaisimka, na miale  yake butu,
Haitakuja zimika, wala kuja shika kutu.

Kama mtu anacheka, meno yake ya  kung’aa,
Siku jua likiwaka, waweza ukazubaa,
Wengi wameweweseka, kuiona hii taa.

Ulaya na Amerika, sifa zake zasikika,
Wametamani kufika, nao wakasuuzika,
Wachache waliofika,wamependa Afrika,

Nami nilihamanika, awali nilipoona,
Homa iliyonishika, walai sikuiona
Kweli niliweweseka, ile taa kuiona.

Ndoto zilikamilika, kwa watu nilijivuna,
Kuishika nilitaka, japo ipo juu sana,
Nguvu ziliongezeka, kila nilipoiona.

Picha ndani nimeweka, wanangu waje ziona,
Yeyote akizitaka, nitampa kuziona,
Na yeye nitamtaka, aende haraka sana.

Twende bila ya kuchoka, ili iwe kumbukumbu,
Hata wao wakifika, wasitwone mambumbumbu,
Waijue Afrika, si bara la mbumbumbu,

Hii taa itawaka,tukitunza kwa makini,
Mafuta haitataka, babda wetu umakini,
Tuipitishe miaka, wabaki waitamani,

Hii taa inawaka ,tuitunze vema sana,
Mwangaza ukitoweka, tutalaumiwa sana,
Majirani watacheka, aibu tutaiona.

Comments

Popular posts from this blog

NOTES ZA USHAIRI

USHAIRI     NI    NINI ? Shaaban Robert katika uandishi wa ushairi ameandika Tenzi na mashairi ya kimapokeo. Tenzi : Ni aina ya mashairi ya kimapokeo wenye sifa zifuatazo: Kimaudhui ; Ni utungo wenye maudhui yanayosimulia kwa urefu tukio fulani maalum. Waweza kuwa wasifu wa mtu au jambo la kihistoria. Mfano; S. Robert ameandika utenzi wa vita vya Uhuru, ameeleza kuhusu historia. Pia katika Mapenzi Bora, ameeleza kuhusu sifa za mapenzi bora. Utenzi ni utungo wa pili kati tungo za ushairi zenye beti nyingi. Utungo wa kwanza unaoongoza kuwa na beti nyingi kuliko zote katika ushairi ni Tendi. Lakini hapa tutaangazia tenzi zaidi. Utenzi hauna mizani nyingi aghalabu mizani nane, hauna mshororo bali una nusu mshororo/kipande mstari. Vilevile katika utenzi kipande mstari hakigawiki. Pia katika kipande mshororo kuna vipande vinne kwa kila ubeti. Mistari mitatu ya kwanza huwa na vina vyenye urari na kipande mstari cha mwisho/cha nne huwa...

Mpangilio wa sura katika utafiti

MADHARA YA MATUMIZI YA KARATASI ZA OMR KATIKA KUJIBIA MITIHANI. Na LEONARD RENATUS, 0759392855 Tasinifu hii ni kwa Ajili ya Kukamilisha Masharti ya  kukamilisha  Stashahada ya elimu ya msingi Chuo cha Ualimu Marangu. SURA YA KWAZA UTANGULIZI Utafiti huu umekusudia kuchunguza madhara na changamoto zitokanazo na karatasi za OMR  katika kujibia mitihani inayotolewa na baraza la matihani Tanzania (NECTA) . Katika sura hii utafiti huu utaangalia vipengele vifuatavyo:- Utangulizi. Usuli wa tatizo. Tamko la utafiti. Lengo kuu la utafiti. Malengo mahsusi yautafiti. Umuhimu wa utafiti. Mawanda ya utafiti. Tafsiri za istlahi zilizotumika 1.2    USULI WA TATIZO OMR ni kifupi cha maneno ya Optical Mark Reader ni mashine ambayo inatumika kusahihishia karatasi za wanafunzi waliofanya mitihani. Kwa hapa Tanzania karatasi hizi hutumika katika kujibia mitihani ya kumaliza elimu ya msingi kwa darasa la saba . Njia hii ya kusahihishia miti...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

Mbinu za kufundishia , ni miongozo mbalimbali atumiayo mwalimu wakati wa kufundisha somo aliloliandaa kwa wanafunzi wake. Walimu wanapaswa kuamua kwa kuchagua kwa makini njia na mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Ziko njia nyingi za kutengeneza mazingira ya mtoto aweze kujifunza na pia ziko mbinu nyingi za kufundishia. Pamoja na wingi huo tunaweza kuzigawa katika makundi makuu mawili kadri ya jinsi zinavyowashirikisha watoto katika tendo la kujifunza, ambazo tunaweza kuziita shirikishi na zisizo shirikishi . Zifuatazo ni baadhi ya mbinu shirikishi na zisizo shirikishi za kufundishia pamoja na faida na hasara zake:- Njia ya majadiliano , njia hii imekuwa ikitumika katika ufundishaji kwa muda mrefu. Katika kujadiliana mwanafunzi mmoja mmoja hupata nafasi ya mawazo aliyonayo kuhusu suala linalojadiliwa na yeye pia huweza kupata mawazo yaw engine. Katika majadiliano mwanafunzi hupata ujuzi mpya nje na ule aliokuwa nao kabla hajashiriki kat...