Skip to main content

SHAIRI: NISEME NINI UJE KWANGU


Kila nikifikiria,ninashindwa kuamua,
Sawa ningevumilia,ila penzi lasumbua,
Kipi sijamwambia,pendo langu kulijua,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Neno nimeshachelewa,lanifanya nikose nguvu,
Hasa ninapogunduwa,kisa ni uvumilivu,
Ni kweli hakuelewa,ishara zangu na wivu,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Sasa nina taabika,na pendo langu hewani,
Si mchezo nateseka,kasema lirudi ndani,
Nashindwa hata kucheka,sipo tena furahani,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Rafiki niseme nini,huyu mtu aje kwangu,
Najua haniamini,atesa fikira zangu,
Mwambie aniamini,mawazo yarudi kwangu.
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Mwambie napenda Mori,sina utani kwa hili,
Leo mie sina gari,kwenye gari siyo mbali,
Nikikosa nina sori,ya kizungu na kiswahili,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Pia mwambie ukweli,wengi wanamtamani,
Hawajui yake hali,wao wapenda kimini,
Tatizo la wake mwili,wakijua hataamini,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Wengi nimeshawaona,wakilia kwa uchungu,
Na ngumu sana kupona,wabaki kusema Mungu,
Sipendi kwake kuona,aje kukufuru Mungu,
Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu.

Kaditama ninatua,uufikishe ujumbe,
Mie moyo waugua,sina nguvu hata chembe,
Awai kumgundua,yule wake kama wembe,
Ataumizwa na kulizwa,nipo chaguo lake.

Comments

Popular posts from this blog

NOTES ZA USHAIRI

USHAIRI     NI    NINI ? Shaaban Robert katika uandishi wa ushairi ameandika Tenzi na mashairi ya kimapokeo. Tenzi : Ni aina ya mashairi ya kimapokeo wenye sifa zifuatazo: Kimaudhui ; Ni utungo wenye maudhui yanayosimulia kwa urefu tukio fulani maalum. Waweza kuwa wasifu wa mtu au jambo la kihistoria. Mfano; S. Robert ameandika utenzi wa vita vya Uhuru, ameeleza kuhusu historia. Pia katika Mapenzi Bora, ameeleza kuhusu sifa za mapenzi bora. Utenzi ni utungo wa pili kati tungo za ushairi zenye beti nyingi. Utungo wa kwanza unaoongoza kuwa na beti nyingi kuliko zote katika ushairi ni Tendi. Lakini hapa tutaangazia tenzi zaidi. Utenzi hauna mizani nyingi aghalabu mizani nane, hauna mshororo bali una nusu mshororo/kipande mstari. Vilevile katika utenzi kipande mstari hakigawiki. Pia katika kipande mshororo kuna vipande vinne kwa kila ubeti. Mistari mitatu ya kwanza huwa na vina vyenye urari na kipande mstari cha mwisho/cha nne huwa...

Mpangilio wa sura katika utafiti

MADHARA YA MATUMIZI YA KARATASI ZA OMR KATIKA KUJIBIA MITIHANI. Na LEONARD RENATUS, 0759392855 Tasinifu hii ni kwa Ajili ya Kukamilisha Masharti ya  kukamilisha  Stashahada ya elimu ya msingi Chuo cha Ualimu Marangu. SURA YA KWAZA UTANGULIZI Utafiti huu umekusudia kuchunguza madhara na changamoto zitokanazo na karatasi za OMR  katika kujibia mitihani inayotolewa na baraza la matihani Tanzania (NECTA) . Katika sura hii utafiti huu utaangalia vipengele vifuatavyo:- Utangulizi. Usuli wa tatizo. Tamko la utafiti. Lengo kuu la utafiti. Malengo mahsusi yautafiti. Umuhimu wa utafiti. Mawanda ya utafiti. Tafsiri za istlahi zilizotumika 1.2    USULI WA TATIZO OMR ni kifupi cha maneno ya Optical Mark Reader ni mashine ambayo inatumika kusahihishia karatasi za wanafunzi waliofanya mitihani. Kwa hapa Tanzania karatasi hizi hutumika katika kujibia mitihani ya kumaliza elimu ya msingi kwa darasa la saba . Njia hii ya kusahihishia miti...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

Mbinu za kufundishia , ni miongozo mbalimbali atumiayo mwalimu wakati wa kufundisha somo aliloliandaa kwa wanafunzi wake. Walimu wanapaswa kuamua kwa kuchagua kwa makini njia na mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Ziko njia nyingi za kutengeneza mazingira ya mtoto aweze kujifunza na pia ziko mbinu nyingi za kufundishia. Pamoja na wingi huo tunaweza kuzigawa katika makundi makuu mawili kadri ya jinsi zinavyowashirikisha watoto katika tendo la kujifunza, ambazo tunaweza kuziita shirikishi na zisizo shirikishi . Zifuatazo ni baadhi ya mbinu shirikishi na zisizo shirikishi za kufundishia pamoja na faida na hasara zake:- Njia ya majadiliano , njia hii imekuwa ikitumika katika ufundishaji kwa muda mrefu. Katika kujadiliana mwanafunzi mmoja mmoja hupata nafasi ya mawazo aliyonayo kuhusu suala linalojadiliwa na yeye pia huweza kupata mawazo yaw engine. Katika majadiliano mwanafunzi hupata ujuzi mpya nje na ule aliokuwa nao kabla hajashiriki kat...