Habarini marafiki,mlofunga hongereni, Nitakuwa mnafiki,nikijifanya sioni, Siyo ishara ya dhiki,bali mwongozo wa dini, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Wagonjwa na wengineo,mlioshindwa kufunga, Myafanye megineyo,itakavyo yenu funga, Sio kucheka wenzio,eti yule hakufunga, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Wewe usiye husika,naomba acha makwazo, Sije mtu kwazika,wewe ukawa ni chanzo, Mtu dini kaishika,kwako liwe kubwa funzo, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Na humu mitandaoni,si sehemu ya dhihaka, Eti nani simuoni,siyo lazima kwandika, Si mtafute simuni,siyo humu kuanika, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Pia ule unafiki,kujifanya umefunga, Waenda kwa marafiki,kuharibu yako funga, Mola hilo haafiki,ni bora usingefunga, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo. Liombeeni taifa,msisahau dunia, Tuyaepuka maafa,mola atawasikia, Pia wale walokufa,huko naijeria, Zaidi ya kutokula,funga ina mengi mambo.... |
KISWAHILI Form 1 Topic 4 FASIHI SIMULIZI Fasihi simulizi ni moja kati ya tanzu za fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo. Katika mada hii utajifunza na kisha utaweza kubainisha tanzu na vipera vya fasihi simulizi pamoja na ufafanuzi wake. Na pia utaweza kutofautisha kati ya kipera na kipera au kati ya utanzu na utanzu. Ubainishaji wa Tanzu za Fasihi Simulizi Tanzu za Fasihi Simulizi Bainisha tanzu za fasihi simulizi Fasihi Simulizi ni kazi ya fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo kama vile; hadithi, ngoma na vitendawili. Tanzu za Fasihi Simulizi ni pamoja na hizi zifuatazo: Masimulizi/hadithi Semi Ushairi Mazungumzo Maigizo Ngomezi Ufafanuzi wa Vipera vya Tanzu za Fasihi Simulizi Vipera vya Hadithi Fafanua vipera vya hadithi SIMULIZI/ HADITHI Masimulizi ni fasihi yenye kusimulia habari fulan...
Comments
Post a Comment