Lugha haina uhusiano wowote na jamii, hali kadhalika jamii haina uhusiano wowote na lugha. jadili.



SWALI.
“Lugha haina uhusiano wowote na jamii hali kadhalika jamii haina uhusiano wowote na lugha”. Jadili kauli hii.



Lugha; ni mfumo wa sauti za nasibu zilizokua katika mpango maalumu na zilizokubaliwa na jamii ya watu fulani ili zitumike katika mawasiliano.

TUKI (2013),kamusi ya Kiswahili sanifu,
 Lugha ni mpangilio wa sauti na maneno unaoleta maana ambao hutumiwa na watu wa taifa au kundi fulani kwa ajili ya mawasiliano. Lugha ni maneno pamoja na matumizi yake.

Jamii ni mkusanyiko wa watu wanaoishi kwa pamoja katika eneo moja la kijiographia wakiunganishwa na historia yao na wakitambuliwa kwa utamaaduni wao,lugha, mila na desturi, 

Uhusiano ni hali ya ukalibu ujirani, urafiki au ushirikiano unaojengeka baina ya ndugu , jamaa au marafiki. Uhusiano ni hali ya kuwa pamoja kifikira ,kimwili kimawasiliano , kiimani, kimaendeleo, kikazi, kijamii na kimichezo. 

Hakuna ukweli wowete kuhusu kauli isemayo kwamba’’ lugha haina uhusiano wowote na jamii , hali kadhalika jamii haina uhusiano woote na lugha’’  bali kuna uhusiano mkubwa unaojitokeza baina ya pande hizi mbili kama ifuatavyo:-

Lugha ni zao la jamii, kwani chanzo cha lugha ni pale tu binadamu walipoanza kuishi pamoja na kukabiliana na mazingira yao, ambapo binadamu alibuni namna ya kuwasiliana. Kwa upande mwingine lugha  ni sehemu ya utamaduni wa jamii husika pia ni njia inayotumiwa na wanajamii ili kueleza na kusambaza  utamaduni.
Hutambulisha kazi za jamii, katika muktadha  ya shughuli mbalimbaili huwepo istilahi na misamiati anuai ambayo wahusika wa kazi au shughuli hizo hutumia wakati wanaposhughulika. Istilahi na misamiati hiyo huwafanya waonekane kuwa tofauti na wanajamii wanaofanya kazi nyinginezo. Mfano istilahi zinazotumiwa na watu wanaofanya kazi hotelini (chai mbili, wali ng’ombe), hospitalini (mbili kutwa mara tatu kwa siku tatu yaani - 23, wachungaji au mashekhe (bwana Yesu asifiwe, assallam-alleikum, tak-biir)  na makuli (lugha za matusi). Lugha hizi hufanya hata watu wengine watambue shughuli zao. 

Lugha hurejelea mazingira ya jamii husika, lugha ina tabia ya kurejelea au kusadifu mazingira halisi ya jamii fulani aghalabu jamii za pwani, huzungumzia zaidi mazingira ya kipwani kutokana na shughuli zinazofanywa na watu wa pwani kama uvuvi. Kwa mfano mzaramo au mndengeleko wa pwani badala ya kuzungumza lugha zinazohusu uvuvi na michezo ya bao, huzungumza lugha zinazohusu ufugaji awapo umasaini Arusha au usukumani Shinyanga.

Lugha huongoza mawazo ya jamii, kwa kawaida mtu hujenga fikra kichwani kwa kutumia lugha. Aghalabu wazo hilo analolifikiria huundwa kwa lugha yake ya msingi, kwa mantiki hiyo hata mtu akiwa mahili wa lugha zaidi ya moja huanza kujenga wazo kwa lugha yake ya kwanza ndipo alitoe wazo hilo kwa lugha ya pili. Kwa mfano watanzania walio wengi ambao lugha yao ya kwanza ni Kiswahili, huwaza kwa Kiswahili kwanza ndipo awasilishe mawazo yake katika lugha hiyo ngeni.

Luhga huhifadhi amali za jamii, lugha hutumika kutunza mila na desturi ambazo ndizo amali za jamii husika. Katika kazi za kisanaa kama vile fasihi simulizi na fasihi andishi ambapo lugha hutumika kuzielezea amali hizo kupitia aina hizo mbili. Katika tamthiliya ya Kinjekitile inaonesha ni jinsi gani jamii zilivyohusika katika vita ya majimaji, hivyo huonesha historia ya jamii husika.

Lugha ni chombo cha kufundishia jamii, kwa mfano jamii ambazo zinajihusisha na masuala ya jando na unyago, vijana hupewa mafunzo kutokana na jinsia zao. Kwenye unyago vijana wa kike hupewa mafunzo ya jinsi gani ya kuishi na familiya zao, na vijana wa kiume hupewa mafunzo ni jinsi gani ya kuishi na familiya zao.

Lugha huishikamanisha jamii, wanajamii kwa kawaida hutumia lugha katika kufanya ushirikiano kwenye shughuli mbalimbali zihuzo maisha yao ya kila siku. Ni katika shughuli za  nyanja zote za maisha, yaani; kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni,na hata kiitikadi kwa kawaida lugha kama chombo cha mawasiliano ndiyo inayowafanya kushirikiana au kushikamana. Kwa mfano wanasiasa katika majukwaa ya kampeni hutumia lugha kuwaalika watu wakusanyike na  kuwaomba wawapigie kura wakati wa uchaguzi, pia katika mikusanyiko ya kidini lugha ndiyo inayowakusanya na kuwashikamanisha wanajamii katika suala hilo la kiitikadi.

Lugha hutambulisha jamii, wanajamii wengi huathiriwa na lugha zao mama hususani lafudhi. Yaani hatakama mwanajamii atakuwa anajua na kutumia lugha zaidi ya moja kwa kawaida hujikuta akitumia lafudhi yake  ya lugha mama kuzungumzia lugha nyinginezo. Jambo hili huwafanya watu hawa kutambulika hata wanapofanya mazungumzo na watu wengine wasio wa makabila yao. Mfano wasukuma, wachaga, wahaya, wamakonde na wamasai hujulikana wanapozungumza  hata na watu wasio wa makabila hayo.

Lugha hurithisha mila na desturi za jamii, hii ni kutokana na baadhi ya tamaduni za jamii husika kutumia lugha kuwafundisha au kuwapa elimu vijana wa jamii hiyo waweze kutambua mila na desturi za jamii yao. Kupitia lugha vijana huweza kutambua masuala mbalimbali yanayowahusu hasa yanayofaa kutendwa na jamii yao na yapi yasiofaa kutendwa na jamii yao. Kwa mfano baadhi ya makabila huwakataza watoto wao wasioe au kuolewa na kabila fulani kwa sababu mbalimbali wanazozijua wao.

Kwa ujumla lugha haiwezi kutenganishwa na jamii hata kidogo, hii ni kutokana na lugha kuwa muhimili ulio imara wa jamii. Kwa hivyo yaweza kusemwa kuwa, bila lugha jamii haiwezi kuwepo kwa kuwa lugha hutumika katika suala zima la kujenga jamii. Kwa mfano jamii ya watu wa afrika mashariki pengine isingekuwepo kama kusingekuwa na lugha ya kuwafanya wawe jamii. 






           




MAREJELEO.
Ø  King’ei, K. (2010). Misingi ya isimu jamii. Taasisi ya taaluma za Kiswahili: chuo kikuu cha Dar es salaam. Tanzania.

Comments

Popular posts from this blog

NOTES ZA USHAIRI

MBINU ZA KUFUNDISHIA

DHANA YA USHAIRI ILIVYOFAFANULIWA NA WATAALAMU MBALIMBALI