Skip to main content

SHAIRI: IWE CHUNGU IWE TAMU

Kwetu ulimi maneno,mengine ni ya ziada,
Siye twatoa misemo,na nyimbo kwenye ibada,
Ladha kwetu siyo somo,ladha kwetu siyo shida,
Iwe chungu iwe tamu,cha msingi ni kushiba.


Vya maana twaviona,twanusa na kusikia,
Hizo suti za kushona,na vingi vya kuvutia,
Tulivitamani sana,tumeshindwa kufikia,
Iwe chungu iwe tamu, cha msingi ni kushiba.

Iwe biringanya mbichi,ama pilipili manga,
Karoti ama kabichi,ama dagaa mchanga,
Sie milo haichoshi,tunatamani kusonga,
Iwe chungu iwe tamu,cha msingi ni kushiba.

Sie hatuna ratiba,tupatacho tunakula,
Tunachopenda kushiba,hatuchagui vyakula,
Bila soda tunashiba,tunakula kisha sala,
Iwe chungu iwe tamu,cha msingi ni kushiba.

Kwetu hatuna jokofu,hatuchachishi viporo,
'Tabaki na yako hofu,utumbo hauna kasoro,
Kunenepa hatuhofu,leo twala kesho doro,
Iwe chungu iwe tamu,cha msingi ni kushiba.

Si kwamba hatutamani,tamaa twaweka ndani,
Twapiga kazi jamani,siku tuwe na vyetu ndani,
Maisha hatulingani,tajiri na masikini,
Iwe chungu iwe tamu,cha msingi ni kushiba.

Shughuli na matukio,twajua chungu na tamu,
Jaani ndo kimbilio,kama vile si timamu,
Njaa huleta kilio,hatujui neno hamu,
Iwe chungu iwe tamu,cha msingi ni kushiba.

Comments

Popular posts from this blog

KISWAHILI FORM 1: FASIHI SIMULIZI

KISWAHILI Form 1 Topic 4 FASIHI SIMULIZI Fasihi simulizi ni moja kati ya tanzu za fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo. Katika mada hii utajifunza na kisha utaweza kubainisha tanzu na vipera vya fasihi simulizi pamoja na ufafanuzi wake. Na pia utaweza kutofautisha kati ya kipera na kipera au kati ya utanzu na utanzu. Ubainishaji wa Tanzu za Fasihi Simulizi Tanzu za Fasihi Simulizi Bainisha tanzu za fasihi simulizi Fasihi Simulizi ni kazi ya fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo kama vile; hadithi, ngoma na vitendawili. Tanzu za Fasihi Simulizi ni pamoja na hizi zifuatazo: Masimulizi/hadithi Semi Ushairi Mazungumzo Maigizo Ngomezi Ufafanuzi wa Vipera vya Tanzu za Fasihi Simulizi Vipera vya Hadithi Fafanua vipera vya hadithi SIMULIZI/ HADITHI Masimulizi ni fasihi yenye kusimulia habari fulan...

MBINU ZA KUFUNDISHIA

Mbinu za kufundishia , ni miongozo mbalimbali atumiayo mwalimu wakati wa kufundisha somo aliloliandaa kwa wanafunzi wake. Walimu wanapaswa kuamua kwa kuchagua kwa makini njia na mbinu bora za kufundishia ili wanafunzi wake waweze kujifunza kwa ufanisi. Ziko njia nyingi za kutengeneza mazingira ya mtoto aweze kujifunza na pia ziko mbinu nyingi za kufundishia. Pamoja na wingi huo tunaweza kuzigawa katika makundi makuu mawili kadri ya jinsi zinavyowashirikisha watoto katika tendo la kujifunza, ambazo tunaweza kuziita shirikishi na zisizo shirikishi . Zifuatazo ni baadhi ya mbinu shirikishi na zisizo shirikishi za kufundishia pamoja na faida na hasara zake:- Njia ya majadiliano , njia hii imekuwa ikitumika katika ufundishaji kwa muda mrefu. Katika kujadiliana mwanafunzi mmoja mmoja hupata nafasi ya mawazo aliyonayo kuhusu suala linalojadiliwa na yeye pia huweza kupata mawazo yaw engine. Katika majadiliano mwanafunzi hupata ujuzi mpya nje na ule aliokuwa nao kabla hajashiriki kat...

DHANA YA USHAIRI ILIVYOFAFANULIWA NA WATAALAMU MBALIMBALI

Ushairi kama moja kati ya tanzu za fasihi inayowasilishwa katika namna zote aidha kwa lugha ya maandishi au kwa lugha ya masimulizi una mchango au nafasi kubwa sana katika kunufaisha au kustawisha maisha ya binadamu kwa kumuelimisha, kumsisimua, kutunza na kuhifadhi amali zake pamoja na kukuza na kuendeleza lugha yake kama moja kati ya vipengere muhimu maishani mwake. Ushairi kama nudhumu katika fasihi simulizi hujumuisha nyimbo, ngonjera, tenzi na mashairi yenyewe. Ushairi wa Kiswahili waweza kuainishwa katika tanzu au katika kumbo mbalimbli kama asemavyo Mulokozi (1996) kuwa zipo kumbo kuu tatu ambazo ni ushairi wa kijadi au kimapokeo, ushairi wa mlegezo au huru na ushairi wa maigizo. Wanazuoni wafuatao wa mashairi ya kimapokeo wametoa maana za ushairi kama ifuatavyo:- Shaaban Robert (1958:37). “Ushairi ni sanaa inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi. Zaidi ya kuwa na sanaa ya vina, ushairi una ufasaha wa maneno machache au muhtasari…, mawazo, maoni na fikra za ndani zi...