SHAIRI: NAHITAJI JIBU LAKO
Zimepita siku nyingi,mori nanze kuandika,
Nilivyoweka ni vingi,hadi kusoma mwachoka,
Hadithi za mitomingi,na visa hadi mwacheka,
Mashairi na hadithi,kipi mimi nakiweza.
Nilivyoweka ni vingi,hadi kusoma mwachoka,
Hadithi za mitomingi,na visa hadi mwacheka,
Mashairi na hadithi,kipi mimi nakiweza.
Sije kuwa kichekesho,kila siku mi nikeshe,
Leo kwenu iwe mwisho,riwaye nikaziache,
Mashairi na hadithi, kipi mimi nakiweza.
Kama naweza kimoja,semeni nisijichoshe,
Mori nisiwe kioja,siku zote nisikeshe,
Nilishike langu moja,roho zenu nizikoshe,
Mashairi na hadithi,kipi mimi nakiweza.
Mashairi nayapenda,niyasome ya wenzangu,
Nazo hadithi napenda,nifanyaje ndugu zangu,
Napenda mkiniponda,nijue kipi fani yangu,
Mashairi na hadithi,kipi mimi nakiweza.
Msomeni kaka nyemo,ama omari maguza,
Tuseme tulikuwemo,ila hatukuongoza,
Wao wamenipa somo,maarifa kuongeza,
Mashairi na hadithi,kipi mimi nakiweza.
Kama vyo naviweza,ndugu mniambieni,
Ukiweza nipongeza,niambie hapa chini,
Muda nisijepoteza,kuwaza niweke nini,
Mashairi na hadithi kipi mimi nakiweza?
Leo kwenu iwe mwisho,riwaye nikaziache,
Mashairi na hadithi, kipi mimi nakiweza.
Kama naweza kimoja,semeni nisijichoshe,
Mori nisiwe kioja,siku zote nisikeshe,
Nilishike langu moja,roho zenu nizikoshe,
Mashairi na hadithi,kipi mimi nakiweza.
Mashairi nayapenda,niyasome ya wenzangu,
Nazo hadithi napenda,nifanyaje ndugu zangu,
Napenda mkiniponda,nijue kipi fani yangu,
Mashairi na hadithi,kipi mimi nakiweza.
Msomeni kaka nyemo,ama omari maguza,
Tuseme tulikuwemo,ila hatukuongoza,
Wao wamenipa somo,maarifa kuongeza,
Mashairi na hadithi,kipi mimi nakiweza.
Kama vyo naviweza,ndugu mniambieni,
Ukiweza nipongeza,niambie hapa chini,
Muda nisijepoteza,kuwaza niweke nini,
Mashairi na hadithi kipi mimi nakiweza?
Comments
Post a Comment