Posts

SHAIRI: NI TAA YA AFRICA

Yang'aa kila dakika, na kuburudisha moyo, Wachache waaliofika, umewatoka uchoyo, Yeyote atamwalika, akaliwazike moyo, Hii taa ya labuka, kaiweka hapa kwetu, Ni kama kaisimka, na miale    yake butu, Haitakuja zimika, wala kuja shika kutu. Kama mtu anacheka, meno yake ya    kung’aa, Siku jua likiwaka, waweza ukazubaa, Wengi wameweweseka, kuiona hii taa. Ulaya na Amerika, sifa zake zasikika, Wametamani kufika, nao wakasuuzika, Wachache waliofika,wamependa Afrika, Nami nilihamanika, awali nilipoona, Homa iliyonishika, walai sikuiona Kweli niliweweseka, ile taa kuiona. Ndoto zilikamilika, kwa watu nilijivuna, Kuishika nilitaka, japo ipo juu sana, Nguvu ziliongezeka, kila nilipoiona. Picha ndani nimeweka, wanangu waje ziona, Yeyote akizitaka, nitampa kuziona, Na yeye nitamtaka, aende haraka sana. Twende bila ya kuchoka, ili iwe kumbukumbu, Hata wao wakifika, wasitwone mambumbumbu, Waijue Afrika, si bara la mbumbumbu, Hii t

HAPPY BIRTHDAY TO YOU

MUNGU AKUPE HEKIMA Miaka mingi imepita,tangu uziache nepi, Hekima umezichota,na kuyaacha makapi, Na mengi umeyapita,sijui myaka mingapi, Mungu akupe hekima,kaka yangu Tumsifu. Kama vile jina lako,Mungu wetu twamsifu, Mema yote yaje kwako,na ujazwe utukufu, Pongezi za ndugu zako,kamwe zisije kukifu, Mungu akupe hekima,kaka yangu Tumsifu. Mama amepata mwana,mwana mwema naamini, Hasemi mtundu sana,bali unajiamini, Wewe kaka ndiwe shina,nduguzo twakuamini, Mungu akupe hekima,kaka yangu Tumsifu. Baba anajivunia,kuwa nawe kila siku, Kwa watu kujisifia,atamani uwe huku, Kakangu unatulia,huna papara za kuku, Mungu akupe hekima,kaka yangu Tumsifu. Mwisho njoo kalamuni,wataka vitu jamani, Wakutaka hadithini,ubuni picha jamani, Wasema uje ubuni,ukuze yako thamani, Mungu akupe hekima,kaka yangu Tumsifu

SHAIRI: NMPE NINI MAMANGU?

Alin i lea mapema,kabla ya kuona jua, Ninamheshimu mama,kweli nimemsumbua, Hadi leo nasimama,na kuongea najua, Mama nitakuheshimu,umefanya mengi kwangu. Usiku haukulala,mie waniangalia, Waja kujua hujala,wengine wamesinzia, Mie nikigalagala,shuka lako nafunua, Mama ninakushukuru,sijui nikupe nini. Mama wewe unapika,mie kukaa sipendi, Mama yangu umechoka, mie kulia  hupendi, Mama umeshughulika,mama wewe ni mshindi, Mama wewe ni shujaa,mola anakutambua. Baba karudi usiku,wewe wamfungulia, Kanywa pombe wamshuku,ila hujamnunia, Huko amekula kuku,wengine kanunulia, Mama umevumilia,ushindi utakujia. Leo baba hanywi pombe,na pia akusifia, Kimwona ana kikombe,maziwa anajinywea, Kikumbuka usiombe,baba yangu atalia, Mama nikulipe nini,ishi nami siku zote. Mama unachechemea,ulipigwa wanambia, Kweli sikutegemea,mama unavumilia, Mungu wamtegemea,muumba waniambia, Mama umebarikiwa,mbinguni tapokelewa. Si kwamba nakusifia,baba nimemchukia, Yeye pia kanilea,siwezi kumchukia,

SHAIRI: KUMBUKUMB YA HAYATI MORINGE SOKOINE

Image
LEO UNGEKUWA NANI? Sasa miongo mitatu,wajina hatukuoni, Wanalalamika watu,kama wewe hawamwoni, Kuvaa vyako viatu,katu haiwezekani, Leo ungekuwa nani,Moringe wa sokoine, Wengi wasema raisi,wa muungano wetu, Eti nawe ungeasi,kukiacha chama chetu, Angekuona raisi,utunge katiba yetu, Leo ungekuwa nani,Moringe wa sokoine. Alokufwata monduli,tunaambiwa fisadi, Chamani hawamjali,yuko bize na miradi, Ilikuua ajali,kukukosa ilibidi, Leo ungekuwa nani,Moringe wa sokoine. Nimefika morogoro,ulipopata ajali, Kule kuna mogogoro,leo ardhi mali, Ninapatwa na kihoro,kuhusu yako ajali, Leo ungekuwa nani,Moringe wa sokoine. Nitakuja kutazama,mahali ulipolala, Kisha nende Butiama,nyerere alipolala, Moyoni inanichoma,sijakuona mahala, Leo ungekuwa nani,Moringe wasokoine. Najuta sijakuona,mie wale wa tisini, Nimepewa lako jina,nalitumia shuleni, Kwenye picha nakuona,nimetunza chumbani, Ulazwe pema peponi,Moringe wa jina wangu......

SHAIRI: U WAPI UJITOKEZA

Nakukumbuka kwa jina,kisa mama,alikwita, Si Jojina Saraphina,Sarah pia aliita, Mora moja nilikwona,siku kwenu ninapita, Uwapi ujitokeze,walisema upo Dar. Nilibadili na njia,kisa kwenu kupapita, Jina lililipatia,kumbe nawe ulipita, Wenyeji nawasumbua,hadi mwizi wananita, U wapi ujitokeze,walisema upo Dar. Walijua twajuana,hata jina nikakwita, Sikuwa makini sana,japo moyo ulipwita, Nilijua ningekwona,nikirudi nakukuta, U wapi ujitokeze,walisema upo Dar. Kwa yeyote ajuaye,alipo wangu muhibu, Aseme alipo yeye,kila swali nitajibu, Katoka Njombe yeye,mtoto wa baba bubu, U wapi ujitokeze,walisema upo Dar. Rangi maji ya kunde,urefu wa wastani, Nywele lazima upende,kope hadi natamani, Jino la mbele upande,na kamwanya ka thamani, U wapi ujitokeze,walisema upo Dar. Kama umeshaolewa,Sarah sema nitambue, Nijuwe nimechelewa,ili nisikusumbue, Mwenzako ni muelewa,sema moyo uamue, U wapi ujitokeze,walisema upo Dar. Kama bado njoo kwangu,sina mwingine banati, Hutoupata uchungu,mwenyewe tapiga goti

SHAIRI: NISEME NINI UJE KWANGU

Image
Kila nikifikiria,ninashindwa kuamua, Sawa ningevumilia,ila penzi lasumbua, Kipi sijamwambia,pendo langu kulijua, Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu. Neno nimeshachelewa,lanifanya nikose nguvu, Hasa ninapogunduwa,kisa ni uvumilivu, Ni kweli hakuelewa,ishara zangu na wivu, Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu. Sasa nina taabika,na pendo langu hewani, Si mchezo nateseka,kasema lirudi ndani, Nashindwa hata kucheka,sipo tena furahani, Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu. Rafiki niseme nini,huyu mtu aje kwangu, Najua haniamini,atesa fikira zangu, Mwambie aniamini,mawazo yarudi kwangu. Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu. Mwambie napenda Mori,sina utani kwa hili, Leo mie sina gari,kwenye gari siyo mbali, Nikikosa nina sori,ya kizungu na kiswahili, Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu. Pia mwambie ukweli,wengi wanamtamani, Hawajui yake hali,wao wapenda kimini, Tatizo la wake mwili,wakijua hataamini, Sijui niseme nini, huyo mtu awe wangu. Wengi nime

SHAIRI: NAJUA NIPO SALAMA

Image
Mama asante sana,pole kwa magumu yote, Ninajua twafanana,kuliko viumbe vyote, Siwazi tutagombana,ukinifanya vyovyote, Nipo mikono salama,asante mama mpenzi. Najua umeteseka,kuumwa na kutapika, Pia ulisonononeka,pia ulisikitika, Moyoni ukaniweka,mama hukutikisika, Nipo mikono salama,asante mama mpenzi. Marafiki ulikosa,wengi walipukutika, Waliona kama kosa,wala hukusikitika, Na hukufikiri posa,huruma ulijivika, Nipo mikono salama,asante mama mpenzi. Bibi alinung'unika,kuona mama walia, Uoga hukujivika,kweli ulivumilia, Hujafa hujaumbika,moyo uliuambia, Nipo mikono salama,asante mama mpenzi. Mwili ulipukutika,afya ikanyong'onyea, Uoga ukafunika,huku ukiniombea, Chakula hakikulika,mama ukanitetea, Nipo mikono salama,asante mama mpenzi. Niliihisi faraja,ulipokuwa na baba, Lilibomoka daraja,hukupunguza mahaba, Nikawaza mama naja,wapi yupo wangu baba, Nipo mikono salama,asante mama mpenzi. Ile sauti ya baba,ilinifanya